MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani
Habari

NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu

CHUO Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) kimewataka wananchi kuwaamini wana uwezo , Ujuzi na Vifaa vya kutosha Kutoa Kozi ya urubani ambayo inatolewa chuoni hapo.

Kimesema mara nyingi watu huwa wanahoji kama Chuo kimejiandaa vya kutosha kuweza Kutoa Kozi hiyo.

Akizungumza katika banda la NIT kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, Mkufunzi wa Urubani kutoka chuo hicho, Ashrafa Ramadhan, amesema tayari mafunzo hayo yameanza na wanafunzi wa kwanza kumi wamejiunga, wakiwemo wanawake wanne na wanaume sita.

“Napenda kuwaondoa hofu. Tumejipanga ipasavyo. Tuna vifaa vya kisasa vya kufundishia marubani kabla hawajapanda ndege, na ndege mpya kwa ajili ya mafunzo zipo tayari,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa NIT imewekeza katika miundombinu na teknolojia ya kisasa ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mafunzo bora ya kitaalamu na ya kimataifa huku gharama zikiwa nafuu ikilinganishwa na vyuo vya nje ya nchi.

“Wito wangu kwa vijana ni kuchangamkia fursa hii adhimu. Mafunzo haya yana nafasi kubwa ya ajira na ujasiriamali katika sekta ya usafiri wa anga. Wazazi pia wawaunge mkono watoto wao kuingia kwenye fani hii ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitawaliwa na wageni,” amesema.

 

 

 

Amesema NIT kinatoa rasmi mafunzo ya urubani kwa vitendo kwa vijana wa Kitanzania, huku kikisisitiza kuwa kina vifaa vya kisasa na wataalamu waliobobea katika nyanja hiyo.

“Nawakaribisha vijana kufika kwenye banda letu wapate elimu ya kina kuhusu kozi ya urubani. Mimi ni miongoni mwa wakufunzi kumi waliopo, na tumeshaanza rasmi mafunzo ya urubani chuoni kwetu. Tumejipanga vizuri kuanzia hatua za awali za kufundisha ardhini hadi mafunzo ya angani,” amesema.

Amebainisha kuwa sifa za kujiunga na mafunzo hayo ni kuwa na elimu ya angalao kidato cha nne, na umri wa kuanzia miaka 17.

Hata hivyo, ameeleza kuwa suala la afya, hasa uwezo wa kuona rangi kwa usahihi, ni jambo linalopewa kipaumbele kikubwa kwa wanaotaka kuwa marubani.

Chuo cha NIT kimekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza rasilimali watu katika sekta ya usafirishaji, na kuanzishwa kwa kozi ya urubani ni hatua nyingine muhimu katika kujenga uwezo wa ndani wa wataalamu wa anga nchini.

You Might Also Like

Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki

JOWUTA Yawasilisha Ripoti ya Ukaguzi kwa Msajili

Majaliwa Amwakilisha Rais Samia Kwenye Kilele Cha Siku Ya Utumishi Wa Umma

Wanafunzi Kutoka Veta Kushiriki Mafunzo Japan

EAC Iweke Ushindani Kuongeza Thamani Ya Malighafi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi
Next Article Mchengerwa Apongeza Shule Ya Sekondari Kibaha Kwa Ufaulu Wa Hali Ya Juu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?