MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ndizi, Mchele, Mafuta Vyapanda Bei
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ndizi, Mchele, Mafuta Vyapanda Bei
Habari

Ndizi, Mchele, Mafuta Vyapanda Bei

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
BEI ya bidhaa muhimu za vyakula zimeendelea kupanda nchini, huku mfumuko wa bei wa Taifa ukifikia asilimia 3.4 kwa mwaka ulioishia Agosti 2025, ukilinganishwa na asilimia 3.3 mwezi Julai mwaka huo.
Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), bidhaa zilizochangia kwa kiasi kikubwa ongezeko hilo ni pamoja na mchele, ambao bei yake imepanda kutoka asilimia 7.8 hadi asilimia 10.5, mtama kutoka asilimia 2.1 hadi 5.5, na unga wa mtama kutoka asilimia 6.1 hadi 10.2.
Habari Picha 9301
Aidha, ndizi mbichi za kupikwa zimeonesha ongezeko kubwa zaidi kutoka asilimia 2.7 hadi asilimia 12.0. Mikate nayo imepanda kutoka asilimia 18.8 hadi 19.3, kuku wa kienyeji kutoka asilimia 12.1 hadi 17.1, mayai ya kuku kutoka asilimia 3.9 hadi 6.4, na mafuta ya kupikia kutoka asilimia 5.8 hadi 6.9.
Vilevile, matunda yamepanda kutoka asilimia 3.6 hadi 5.2, huku bei za vinywaji visivyo na kilevi kama juisi na soda zikiongezeka kutoka asilimia 3.3 hadi 3.5.
Kwa upande wa bidhaa zisizo za chakula, taarifa ya NBS inaonesha kuwa sigara zimepanda kutoka asilimia 5.8 hadi 6.0, viatu vya wanawake kutoka asilimia 1.0 hadi 1.6, na viatu vya watoto kutoka asilimia 1.8 hadi 2.2.
Bidhaa za matumizi ya nyumbani pia zimeathirika. Bei ya vitanda imepanda kutoka asilimia 2.2 hadi 3.3, jokofu kutoka asilimia 0.4 hadi 1.5, jiko la umeme kutoka asilimia 1.7 hadi 2.0, na jiko la mkaa kutoka asilimia 7.3 hadi 11.4.
Bei ya vyombo kama sahani imeongezeka kutoka asilimia 3.5 hadi 5.0, vikombe kutoka asilimia 1.9 hadi 2.5, na dawa ya mbu kutoka asilimia 8.5 hadi 9.0.
Kwa upande wa usafiri na teknolojia, pikipiki zimepanda kutoka asilimia 2.7 hadi 3.5, simu za mkononi kutoka asilimia 0.2 hadi 1.5, na kompyuta mpakato kutoka asilimia 3.0 hadi 5.2.
Aidha, bidhaa na huduma zinazohusiana na starehe, michezo na utamaduni nazo zimeonesha ongezeko kutoka asilimia 1.0 hadi 1.4.
Kwa ujumla, mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi umeongezeka hadi asilimia 7.7 kwa mwaka ulioishia Agosti 2025, kutoka asilimia 7.6 mwezi Julai. Vilevile, mfumuko wa bei wa bidhaa zisizo za chakula umeongezeka hadi asilimia 1.6 kutoka 1.5 kwa kipindi kama hicho.
Katika ukanda wa Afrika Mashariki, hali ya mfumuko wa bei imeonesha tofauti. Nchini Uganda, kiwango kimesalia asilimia 3.8 kama kilivyokuwa mwezi Julai, huku nchini Kenya, mfumuko wa bei umeongezeka kutoka asilimia 4.1 hadi 4.5 kwa mwaka ulioishia mwezi huo.

You Might Also Like

Jeshi la polisi kumhoji anayesambaza taarifa za uongo

Watumishi Wanawake Wa TEA wajitoa Kwa Jamii

Senene Waongezewa Thamani UDSM

Matumizi Holela Ya Vilevi Hatari Kwa Watumiaji

GIZ, IUCEA waratibu uchambuzi wa data kidijitali kwa wahitimu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article FCC Yawavutia Wawekezaji Kwenye Maonesho Ya IATF Nchini Algeria
Next Article Balozi Sirro: Bila Amani, Maendeleo Hayapo Kigoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Rais Wa CWT Suleiman Ikomba Sasa Ni Daktari
Habari September 13, 2025
Salum Mwalim: Nitarejesha Hadhi ya Kanda ya Ziwa na Kuinua Zao la Pamba
Habari September 12, 2025
TEA Yatathmini Utekelezaji na Kupanga Mwelekeo Mpya Kupitia Baraza la Wafanyakazi
Habari September 12, 2025
Manara: Sitapambana na Wafanyabiashara, Nitawatetea
Habari September 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?