MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mwenyekiti TCCIA Geita Gabriel Ahamasisha Watanzania Kutumia Bidhaa Za Ndani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mwenyekiti TCCIA Geita Gabriel Ahamasisha Watanzania Kutumia Bidhaa Za Ndani
Habari

Mwenyekiti TCCIA Geita Gabriel Ahamasisha Watanzania Kutumia Bidhaa Za Ndani

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: MWENYEKITI wa Chemba ya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoa wa Geita, Robert Gabriel ameeleza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta ya viwanda, hasa viwanda vya bidhaa za ngozi na nyama nchini Tanzania.
Gabriel ameelezea mafanikio hayo alipozungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya nane ya Sekta ya Madini mkoani Geita.
Amesema uwepo wa viwanda hivyo unathibitisha kuwa Tanzania ya viwanda si ndoto tena bali ni uhalisia unaoonekana.
Habari Picha 9669
Ametoa mfano wa kiwanda cha zamani cha viatu cha Bora, kilichokuwa maarufu enzi za Mwalimu Nyerere, akisema sasa bidhaa zake zimehuishwa kupitia kiwanda cha Kilimanjaro International Leather Industries, kinachozalisha viatu vya ngozi kutoka kwa wanyama walioko nchini Tanzania.
“Leo hii, viatu vya Kilimanjaro Leather ni vya ubora wa kimataifa. Ni imara na vinafaa kwa wanafunzi wa kike na wa kiume. Wazazi wanaojali watoto wao wanapaswa kuvitumia,” amesema Mwenyekiti huyo.
Habari Picha 9670
Ametoa wito kwa wafanyabiashara nchini kuacha kuagiza viatu kutoka nje ya nchi na badala yake watangaze na kuuza bidhaa za ndani ili kusaidia kukuza uchumi, kuongeza ajira na kuchangia mapato ya kodi kwa serikali.
Aidha, ameelezea mafanikio ya kiwanda cha kuchakata nyama kinachomilikiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), kwamba kiwanda hicho hufuga ng’ombe, huchinja,  na kusindika nyama kwa viwango vya kimataifa.
Amesema tayari bidhaa zake zina soko katika nchi mbalimbali zikiwemo Qatar, Saudi Arabia, na mataifa mengine.
Habari Picha 9671
“Tumezoea kula nyama ngumu kwa sababu ya kuchinja wanyama waliodhoofika. Leo hii, Tanzania tuna nyama laini na bora inayozalishwa hapa hapa nchini kwa kiwango cha kimataifa,” amesema.
Akizungumza kwa niaba ya kiwanda cha Kilimanjaro International Leather, Ofisa Mauzo Mwandamizi, Christopher Manyani, amesema bidhaa zao zina ubora wa hali ya juu huku bei zake zikiwa nafuu, kulingana na aina ya viatu.
Amesisitiza kuwa Watanzania wanapaswa kuachana na dhana ya kudhani bidhaa kutoka nje ni bora zaidi.
Kwa upande wake, Noel Tuga, Ofisa Mwandamizi wa Uwekezaji kutoka PSSSF, amesema mfuko huo unaendelea kusimamia kwa karibu miradi ya wanyama na viatu, akisisitiza kuwa viwanda hivyo vina mchango mkubwa katika kuinua uchumi na kuongeza ajira.
Katika maonesho hayo, Chemba ya Wafanyabiashara ilitoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuyawezesha maonesho hayo kufanyika kila mwaka na kwa kuhakikisha maboresho katika sekta ya madini na viwanda yanatekelezwa kwa vitendo.
Mwenyekiti wa Chemba Gabriel amesema, agizo la Rais kuhusu maboresho ya miundombinu limeleta mafanikio makubwa, yakiwemo majengo ya kudumu kwa taasisi mbalimbali, ikiwemo Wizara ya Madini na PSSSF.
Aidha, amesema maonesho hayo yamevutia wageni kutoka nchi za jirani kama Rwanda, Burundi, Sudan ya Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na Kenya, ambao wanashiriki kwa ajili ya fursa za biashara.
“Kama Chemba, tunahakikisha tunakuwa sauti ya makundi yote haya. Tutaendelea kushirikiana na serikali na wadau wengine kuhakikisha mafanikio haya yanaendelezwa,” amesena.

You Might Also Like

Ripoti Ya Bodadoda Yazinduliwa

Tanzania Yaibuka Kidedea Maonesho Zambia

Baraza La Mawaziri La SADC Lahitimisha Kikao Chake Jijini Antananarivo

Ridhiwani, Waziri Wa Kazi, Ajira UAE Waweka mkakati

Silaa: Akili Mnemba, Roboti kuongeza ufanisi,ubunifu 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article NIC Yatoa Elimu ya Bima Kwenye Kijiji cha Bima, Maonesho ya Madini Geita
Next Article BOT Yatoa Elimu ya Uwekezaji, Fedha Kwa Wananchi Maonyesho ya Madini Geita
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?