MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari

MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imewafuata wananchi huko waliko kupitia huduma za kliniki tembezi, njia inayoleta  urahisi wa huduma za afya.
Daktari Bingwa wa upasuaji wa mifupa kutoka MOI, Tumaini Minja amesema hayo wakati wa  Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma.
Amesema kupitia ushiriki wao kwenye maonesho hayo,  MOI imefanikiwa kuhudumia zaidi ya wananchi 70 waliojitokeza kupatiwa huduma za uchunguzi na ushauri wa kitaalamu, hasa kwa magonjwa ya mifupa, nyonga, magoti na mgongo.
“Tumekutana na wananchi wengi waliokuwa wakihitaji huduma maalum ambazo kwa kawaida hupatikana Dar es Salaam pekee.
“Kupitia kliniki hii tembezi, tumewafikia wananchi wa Dodoma na mikoa ya jirani kwa urahisi zaidi, na bado tutaendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi lengo ni kuona wa Tanzania wananufaika na huduma za matibabu kwa urahisi na ufanisi,” amesema.
Amesema lengo la taasisi hiyo, ni kuhakikisha huduma bora za afya ya ubongo, mgongo, mishipa ya fahamu na mifupa zinawafikia Watanzania wote kwa usawa.
 “Tunaendelea kutoa huduma hata baada ya maonesho kumalizika, na tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia na Serikali kwa kutuwezesha kufanya haya kupitia kliniki tembezi inayojumuisha madaktari bingwa mbalimbali,” amesema.
Pia taasisi hiyo inatoa elimu ya afya kwa wananchi ili kusaidia jamii kutambua mapema dalili za maradhi sugu yanayohusiana na mifupa na mgongo, hivyo kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kwa kuchelewa kutafuta tiba.
Amesema huduma hizo za karibu na wananchi zitakuwa endelevu, wametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa kila timu ya madaktari bingwa inapokuwa katika mikoa yao.

“Tumekutana na wananchi wengi waliokuwa wakihitaji huduma maalum ambazo kwa kawaida hupatikana Dar es Salaam pekee,” amesema.

You Might Also Like

Silaa Atembelea Banda La NEMC, Wiki Ya Anwani Za Makazi

Silinde Akabidhi Nyaraka za Kufungua Masoko Mapya Nje ya Nchi

Jeshi la polisi kuchukua tahadhari mechi ya Simba, Yanga leo

Matokeo Ya Usaili TRA Kutangazwa April 25,2025

Watu Milioni 300 Afrika Kutumia Nishati Ya Umeme Ifikapi 2030-Biteko

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Next Article Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Habari June 19, 2025
Serikali Yatumia Zaidi Ya Bilioni 100 Kupeleka Umeme Simiyu
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?