MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa
Habari

Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: KAMPUNI ya Sotta Mining Corporation Ltd inaendelea na ujenzi wa mgodi wa kisasa wa dhahabu katika eneo la Nyanzaga, wilayani Sengerema, mkoani Mwanza, ambapo shughuli hizo zinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka miwili, na uzalishaji wa kwanza wa dhahabu kuanza rasmi ifikapo robo ya kwanza ya mwaka 2027.
Akizungumza kuhusu maendeleo ya mradi huo, Mhandisi Mkuu wa Mradi, Richard Ojendo, amesema tayari nyumba 151 zimejengwa kwa ajili ya wananchi waliopisha mradi huo, huku nyumba nyingine 111 zikiendelea kujengwa na kukamilika ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu.
Habari Picha 9537
Amesema Mradi huo pia unahusisha ujenzi wa kinu cha kuchakata dhahabu, kitakachohusisha shughuli za kusaga na kusigina, kazi ambayo pia itachukua miaka miwili.
Sotta Mining Corporation inamiliki mgodi huo kwa asilimia 80, huku Serikali ya Tanzania ikiwa na umiliki wa asilimia 20.
“Nipo hapa kusimamia mradi huu muhimu kwa taifa. Tuko hatua ya ujenzi wa miundombinu na tunaendelea kuhamasisha wananchi waliokuwa eneo hili kuupisha mradi. Tunajenga kwa viwango vya juu na kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma,” amesema Mhandisi Ojendo.
Habari Picha 9538
Wananchi waliopisha mradi huo wameanza kunufaika na maendeleo yanayoletwa na uwepo wa mgodi huo. Prisca Mapembe, mmoja wa waliojengewa nyumba, amesema maisha yao yamebadilika kwa kiwango kikubwa.
“Awali maisha yalikuwa duni, lakini sasa tumejengewa nyumba bora zenye hadhi, tuna maji safi na salama, umeme umefika, na visima vya maji vimechimbwa. Pia zikitokea nafasi za kazi, tunapewa kipaumbele,” amesema Prisca.
Habari Picha 9539
Kwa upande wake, Felician Bukwimba, mmoja wa vijana walioajiriwa katika shughuli za ujenzi, amesema mgodi huo umekuwa neema kwao.
“Ninajivunia kufanya kazi katika mradi huu. Wazawa tunapewa kipaumbele hasa kwenye kazi kama za utengenezaji wa tofali na nyinginezo. Hii ni fursa ambayo haipatikani kirahisi,” amesema Bukwimba.
Mradi wa Nyanzaga unatarajiwa kuwa moja ya migodi mikubwa ya dhahabu nchini, ukiwa na mchango mkubwa kwenye uchumi wa taifa na kubadili maisha ya wakazi wa maeneo ya jirani.

You Might Also Like

VETA Mikumi Yatengeneza Mashine Ya Kuchakata Majani Ya Mifugo

Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana

Chalamila Atoa Wiki Mbili Wafanyabiashara Ndogo Ndogo Kufungua Njia Kariakoo

NIT Yasema Ina Uwezo Wa Kufundisha Kozi Ya Urubani

Usafirishaji Shehena Waingiza Dola Bilioni 3.54

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa
Next Article Fema Mining & Drilling Mfano wa Kuigwa – Musukuma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchimbi Ahimiza Ushirikiano wa Wizara Katika Uhifadhi wa Mazingira
Habari March 10, 2026
Mtaka, Ndunguru Wakubaliana Ujenzi wa Maabara ya Kimkakati Njombe
Habari March 10, 2026
Wataalamu wa Fedha SADC Wakutana Pretoria Kujadili Bajeti
Habari March 9, 2026
TASFAM Yawawezesha Wanawake wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Kuadhimisha Siku ya Mwanamke
Habari March 9, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?