MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: MATUKIO YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI SASA DISEMBA 2024:
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Makala > MATUKIO YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI SASA DISEMBA 2024:
Makala

MATUKIO YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI SASA DISEMBA 2024:

Author
By Author
Share
5 Min Read

KATIKA kipindi cha mwaka mzima kuanzia Januari 2024, hadi sasa, serikali imekuwa ikijitahidi kuboresha maeneo mbalimbali ili kuleta tija kwa taifa.

Haya ni baadhi ya mafanikio hayo yaliyofanywa na serikali kwa kipindi chote hicho;

JANUARI MOSI, 2024:   Rais Samia Suluhu Hassan alitoa agizo kuwa ikifikia Julai, SGR iwe imeanza.

Samia alitoa agizo hili alipokuwa akiainisha mipango ya serikali kwa mwaka 2024.

JANUARI 10, 2024: SAMIA: Tutatawala soko la karafuu ulimwenguni.

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema serikali kupitia balozi zake na majukwaa mbalimbali yataendelea na jitihada za kufungua masoko ya zao la karafuu ili kuongeza uuzaji wa zao hilo nje ya nchi.

Kiongozi huyo wa nchi ametoa kauli hiyo leo alipozungumza na wananchi katika tukio la azinduzi wa jengo la Kitega Uchumi la Zanzibar State Trade Cooperation – Pemba visiwani Zanzibar.

JANUARI 23, 2024: Nchi ipo salama

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi Tanzania, Jenerali Jacob Mkunda, amethibitisha kuwa amani na usalama wa nchi upo vizuri.

JANUARI 25,2024 Rais samia asifiwa kuimarisha demokrasia

Falsafa yake ya 4R kwa vitendo yagusa wengi, Mbowe ampongeza.

MACHI 12, 2024 Bajeti serikali juu kwa asilimia 11.2

Yafikia sh. Trilioni 49.3, ya sasa mafanikio kibao, sababu uchumi kuimarika zatajwa.

APRILI 27, 2024 Sherehe miaka 60 ya Muungano yafunika

Gwaride, makomandoo, tarabushi vyakonga nyoyo

Viongozi Afrika, Kimataifa Waipa ‘tabo’ Tanzania

Samia aagiza 4R zitekelezwe, uwajibikaji

wafungwa 1,082 wasamehewa

APRILI 30, 2024 Serikali kulipa madeni ya vyombo vya habari

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema atamwambia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Viongozi Wakuu wa serikali wazisihi wizara na Taasisi za Umma kuanza kulipia madeni ya matangazo wanayodaiwa na vyombo vya habari.

Biteko amesema hayo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Kitaaluma wa 13 wa mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania ( TEF), Jijini Dodoma.

MEI 12, 2024 Majaketi yenye camera kudhibiti rushwa trafiki

Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango, ameiagiza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuharakisha mchakato wa matumizi ya majaketi yenye kamera kwa askari wa usalama barabarani, ili kukomesha vitendo vya rushwa ambavyo kwa sehemu, vimekuwa sababu ya ajali.

Dkt. Mpango ameyasema hayo jijini Dodoma, alipokuwa akifungua kituo kipya cha polisi cha daraja ‘A’ cha wilaya ya kipolisi Mtumba pamoja na ugawaji wa magari 21.

JUNI 14, 2024 Safari ya kwanza SGR

Safari ya kwanza ya treni ya umeme (SGR), kutoka Morogoro kwenda Dar es Salaam imeanza rasmi Juni 14, 2024.

Treni hiyo ilianza Safari kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro saa 12 asubuhi na ilifika mkoani humo saa 1:59 asubuhi

JULAI 11, 2024 Mikopo asilimia 10 yaiva

RAIS Samia Suluhu Hassan ametangaza kurejesha tena utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu kuanzia July, 2024 kwa utaratibu wa kutumia Benki kwa Halmashauri 10 za majaribio.

Halmashauri hizo  ni Majiji ya Dar es Salaam na Dodoma, Manispaa za Kigoma Ujiji na Songea, Miji ya Newala na Mbulu, Wilaya za Siha, Nkasi, Itilima na Bumbuli.

Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa ametoa taarifa hiyo Bungeni Jijini Dodoma leo April 16,2024 wakati akitoa hotuba kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2024/2025.

JULAI 16, 2024 Udart kuingiza mabasi 100 mwendokasi

MSAJILI wa Hazina Nehemiah Mchechu amesema Serikali ipo mbioni kuongeza mabasi 100 kwenye Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka

Mabasi hayo mapya yataenda kujikita katika njia kuu tu.

Sambamba na hilo Serikali  yenye umiliki wa asilimia 85 kwenye mradi huo inakwenda kuongeza kampuni nyingine itakayosaidiana na Kampuni ya Usafirishaji ya Mabasi yaendayo Haraka(UDART)katika utoaji huduma

SEPTEMBA 2, 2024 Miaka 60 ya JWTZ – Tuko Imara

Rais Samia Suluhu Hassan, ataja msingi wa uimara wa jeshi na maboresho yaliyofanyika, akitaka matumizi zaidi ya teknolojia.

DISEMBA 24, 2024 Biashara saa 24 Dar mwezi ujao

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila ametangaza kuwa Januari, 2025 utafanyika uzinduzi mkubwa Kariakoo wa biashara Kufanyika masaa 24.

Chalamila ameyasema hayo leo Desemba 23, 2024 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Sikukuu ya Krismas na Mwaka Mpya.

Imeandaliwa na Mwandishi Lucy Ngowi:

You Might Also Like

Mpulla: Serikali Imetekeleza Hoja Za TUCTA Kuiboresha CMA

Akili Bandia Yachochea Ushirikiano Kati Ya China, Afrika

Tujenge Jumuiya Yenye Mustakabali wa Pamoja kati ya China na Afrika – Wang Yi

Matukio ya Wafanyakazi Yaliyojiri kuanzia Januari 2024, Hadi Leo Disemba 31, 2024

Dkt. Biteko Afuta Likizo Za Watumishi Wote Tanesco

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mkurugezi Mkuu LATRA, Kamanda Ng’anzi Wafanya Ukaguzi Wa Kushtukiza Stendi Ya Magufuli
Next Article MATUKIO YA MISIBA KWA WATU MAARUFU YALIYOJIRI KUANZIA JANUARI 2024, HADI DISEMBA 2024
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?