MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa: Elimu Ya Watu Wazima, Silaha Ya Mapinduzi Ya Maendeleo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa: Elimu Ya Watu Wazima, Silaha Ya Mapinduzi Ya Maendeleo
Habari

Majaliwa: Elimu Ya Watu Wazima, Silaha Ya Mapinduzi Ya Maendeleo

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: WAZIRI Mkuu wa Kassim Majaliwa, amesema elimu ya watu wazima ni zaidi ya masomo ya kawaida, pia zana muhimu ya kuleta maendeleo endelevu kwa taifa.
Akizungumza leo Agosti 25, mwaka 2025 alipofungua kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), lililofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Majaliwa  amesema elimu hiyo ina mchango mkubwa katika kuongeza kipato, kuboresha ustawi wa kijamii, afya na ushiriki wa kiraia.
Habari Picha 9117
“Elimu si tukio la muda, bali ni safari endelevu ya kujifunza katika maisha yote. Elimu ya watu wazima haimuhusu mtu mzima pekee, hata vijana wanaweza kujiunga na kunufaika na programu mbalimbali za ujuzi zinazotolewa na taasisi hii,” amesema Majaliwa.
Ameongeza kuwa uzoefu wa kimataifa unaonesha kuwa elimu ya watu wazima ni chombo muhimu katika maendeleo ya kijamii, kiuchumi na binafsi.
Ameipongeza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kwa mchango mkubwa katika kipindi cha nusu karne, hususan katika kutoa elimu nje ya mfumo rasmi na kuwafikia Watanzania waliokuwa hawajapata fursa ya elimu ya msingi.
Habari Picha 9118
“Taasisi hii imekuwa mshauri wa Serikali katika masuala ya kisera na kitaalamu. Imechangia kwa kiasi kikubwa katika kuwafikia makundi yaliyosahaulika kwa muda mrefu,” ameongeza.
Ameielekeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kushirikiana na taasisi hiyo kuongeza upatikanaji wa elimu kwa watu wazima, hasa katika maeneo ya pembezoni na yenye changamoto za kijamii na kijiografia.
Vilevile, ameagiza taasisi hiyo kushirikiana na wadau mbalimbali kufanya tafiti za mara kwa mara ili kubaini changamoto zinazokabili sekta hiyo na kuandaa suluhisho bunifu linalokidhi mahitaji ya jamii.
Habari Picha 9119
Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema  taasisi hiyo imekuwa ikitekeleza miradi mikubwa ya kimkakati, ikiwemo Mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP).
“Kupitia SEQUIP, wasichana 13,272 waliokuwa wameacha shule wameweza kurejea katika mfumo wa elimu ndani ya kipindi cha miaka mitano,” amesema.
Ameongeza kuwa mradi mwingine wa Mpango Jumuishi kwa Vijana Walioko Nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu (IPOSA), umefanikiwa kuwajengea uwezo vijana 10,000 walioko nje ya mfumo rasmi katika maeneo ya stadi za maisha, ujasiriamali na ufundi wa awali.
Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Profesa Philipo Sanga, amesema taasisi yake inajivunia mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya Serikali hususan katika maboresho ya sera ya elimu jumuishi inayolenga kuwafikia Watanzania wote bila ubaguzi.
“Sera hii ya elimu jumuishi imekuwa chachu ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata nafasi ya kujifunza, bila kujali umri, jinsia au hali ya maisha,” amesema.

You Might Also Like

Timu Wizara Ya Nishati Zawasili Tayari Kwa Bonanza

TIB Yaanda Mkakati Kabambe Wanawake Kuchangamkia Fursa

Theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa ipo kwenye kilimo

Waandishi wa Habari wa Afrika wapata mafunzo ya Kuandika Habari za Uhamiaji

JAB Yatoa Mwezi Moja Kuthibitishwa, kupewa vitabulisho

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wafanyakazi Wapongeza Uzinduzi wa Miongozo, Mifumo ya Kielektroniki ya Ofisi ya Waziri Mkuu
Next Article Majaliwa Ataka Wafanyakazi Waandaliwe Kwa Mabadiliko Ya Teknolojia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?