MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato
Habari

Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Mwandishi Wetu
TANGA: WAZIRI wa Madini Anthony Mavunde amesema tangu kufanyika kwa maboresho ya Sheria na Kanuni za Madini kupitia Tume ya Madini, Wizara hiyo imeongeza kasi ya ukusanyaji wa maduhuli kutoka mwaka hadi mwaka.
Mavunde ameyasema hayo katika kikao alichofanya na Menejimenti ya Tume ya Madini, Wakurugenzi, Mameneja na Maofisa Madini wakazi wa mikoa, chenye lengo la kuweka mikakati ya kuimarisha Sekta ya Madini katika kipindi cha mwaka wa fedha 2024/2025.
Uimarishaji huo ni kupitia ukusanyaji wa maduhuli, udhibiti wa utoroshaji wa madini, udhibiti wa mianya ya upotevu wa makusanyo na kuimarisha usalama kwenye shughuli za uchimbaji wa madini.
Amesema siri ya kasi hiyo inatokana na
ubunifu wa ukusanyaji wa maduhuli kwa kudhibiti mianya ya utoroshaji wa madini.
“Niwapongeze kwa kazi nzuri sana ya ukusanyaji wa maduhuli hasa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi sasa ambapo kiasi cha Sh. Bilioni 196 zimekusanywa, kiasi ambacho kinazidi kiasi kilichokusanywa kwa mwaka mzima wa fedha wa mwaka 2015/2016,” amesema.
Kutokana na mafanikio hayo, amesema kiasi hicho cha pesa kilichokusanywa cha sh. Bilioni 196 kwa kipindi cha miezi miwili kwa mwaka wa  fedha 2024/2025 ni zaidi ya kiasi cha Sh. Blioni 161 kilichokusanywa kwa mwaka mzima wa fedha 2015/2016.
Kwa upande mwingine Mavunde ameipongeza serikali kwa kutoa kipaumbele katika sekta hiyo kwa kuongeza bajeti ya wizara hiyo kutoka Sh. Bilioni 89 hadi 231 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025.
“Bajeti hii kubwa tuliyopewa inakwenda kutatua changamoto mbalimbali katika Sekta ya Madini ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vifaa kama vile magari 89 na pikipiki 140 ambazo zitatumika kuyafikia maeneo yote yenye shughuli za uchimbaji wa madini na ukusanyaji wa maduhuli.
Pia ametoa maagizo matano kwa maofisa madini wakazi wa mikoa kutatua kwa haraka migogoro ya wachimbaji wa madini kwa kusimamia haki.
Lingine ni kuimarisha udhibiti wa utoroshaji wa madini kwa kushirikiana na vikosi kazi, vyombo vya ulinzi na usalama na kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato.
Maagizo mengine ni Ofisi ya Kamishna wa Madini kwa kushirikiana na Ofisi za Maofisa Madini Wakazi wa Mikoa kushirikiana kwa pamoja kuwalea, kuwakuza na kuwaendeleza wachimbaji wadogo wa madini.
Naye Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa  amesema kupitia  ushirikishwaji kwa watendaji wa wizara hiyo na taasisi zake, mchango wa sekta hiyo kwenye pato la taifa umeendelea kukua.
Amesema uhakika upo ifikapo mwaka 2025 mchango huo kwenye pato la taifa utafikia asilimia 10.
Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Yahya Samamba amesema wizara na taasisi zake ipo tayari kufanyia kazi maelekezo mazuri yanayoendelea kutolewa lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na rasilimali za madini nchini.
Awali akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Batilda Buriani amesema sekta hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa cha ukusanyaji wa mapato ya mkoa.
Amealika wawekezaji kujitokeza katika mkoa kwa kuwa kuna wingi wa madini ya metali, ujenzi, vito na ya viwandani.
Pia ameomba wachimbaji wadogo  na wakinamama kupewa mitaji na elimu kuhusu uchimbaji wa madini.

You Might Also Like

RC Dodoma Atoa Maagizo Kwa Ma – DC Kuhusu Ukame

Dkt. Bwana: Tunafanya utafiti wa mbegu kutatua changamoto za wakulima

DART Toeni Fursa Kwa Watanzania Kuwekeza kwenye Mwendokasi -Mchengerwa

Majaliwa Asema Sekta ya Uvuvi Yaingiza trilioni 2.9 kwa Mwaka 

BRT Kuimarisha Uhusiano Tanzania, China

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article OUT yaunda Kamati ya Ufuatiliaji na Tathmini Mradi wa HEET
Next Article Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?