MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Maabara Za Sayansi Zachochea Hamasa Kitaaluma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Maabara Za Sayansi Zachochea Hamasa Kitaaluma
Habari

Maabara Za Sayansi Zachochea Hamasa Kitaaluma

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MAABARA za Fizikia, Kemia na Biolojia zilizogharimu Sh. Milioni 180 katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kakonko, Kigoma zimechochea hamasa kubwa ya kitaaluma kwa wanafunzi.
Maabara hizo zimejengwa kwa ufadhili wa Shirika la Watoto Duniani (UNICEF) kwa kushirikiana na Mfuko wa Elimu wa Taifa (TEA). Shule hiyo ina wanafunzi 270 kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne.
Mkuu wa shule ya Kakonko, Anatoria Nkabo, amesema kukamilika kwa mradi huo kutaongeza hamasa ya wanafunzi kufanya vizuri zaidi katika masomo ya sayansi kutokana na mazingira bora na rafiki ya kujifunzia kwa vitendo.
“Kwa kupata mradi huu, tunakwenda kuongeza ufaulu. Tunatarajia nusu ya wanafunzi watakaoingia kidato cha nne wapate daraja la kwanza katika mitihani yao ya mwisho,” amesema.
Mwalimu wa Kemia na Biolojia, Nikolous Kayombo, amesema kuwa walifundisha masomo hayo kwa nadharia pekee, lakini sasa, kupitia maabara hizo wanafunzi wataweza kujifunza kwa vitendo, hivyo kuongeza uelewa na ufaulu wao.
Wanafunzi Zulfa Twaha  wa Kidato cha Kwanza, Happines Amosi (Kidato cha Tatu), na Sharifat Hamad walitoa shukrani zao kwa UNICEF na TEA kwa kuwapatia maabara hizo muhimu.
Walisema maabara hizo zinawawezesha kufanya majaribio mengi ya masomo ya sayansi, jambo linalochochea mafanikio yao kitaaluma.
Mbali na maabara, TEA pia ilitoa ufadhili wa ujenzi wa bweni lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 120 mwaka 2022/2023, kwa gharama ya zaidi ya Sh. milioni 142.9.
Shule  hiyo ilianzishwa mwaka 2022 ina jumla ya wanafunzi 274, na mwaka 2025 inatarajia kudahili wanafunzi wengine 100 wa kidato cha kwanza, jambo linaloashiria maendeleo endelevu shuleni hapo.

You Might Also Like

Watafiti Mataifa 10 Kujadili ElimuMsingi Nchini

TPHPA, KEM Wasaini Hati Ya Makubaliano Udhibiti Viuatilifu

Biteko Akaribisha Wawekezaji Sekta Ya Nishati

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni

Majaliwa: Jiungeni NHIF Kupata Matibabu Ya Uhakika

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waziri Mkuu Majaliwa Amwakilisha Dkt.Mpango Mahafali Ya 43 OUT
Next Article
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?