MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kipanga: Lugha ya Kichina Inakuza Diplomasia, Kuimarisha Uhusiano
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kipanga: Lugha ya Kichina Inakuza Diplomasia, Kuimarisha Uhusiano
Habari

Kipanga: Lugha ya Kichina Inakuza Diplomasia, Kuimarisha Uhusiano

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: NAIBU Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga amesema lugha ya kichina inakuza diplomasia na kuimarisha uhusiano mzuri katika kuwezesha diplomasia ya kiuchumi.

Kipanga amesema hayo kwenye hafla ya Mashindano ya Kimataifa ya Walimu wa Lugha ya Kichina nchini Tanzania yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Amesema lugha hiyo ilianza kufundishwa nchini tangu mwaka 2013 kupitia Taasisi ya Kichina ya UDSM.

Amesema kujifunza lugha hiyo kutafungua milango ya fursa pamoja na mawasiliano rahisi na Wachina katika nyanja mbalimbali.

“Kwa kujihusisha na mawasiliano kama haya, unafungua milango ya maendeleo yako ya elimu, taaluma ya biashara na kukuza utalii wa lugha. Hivyo kutokana na diplomasia ya lugha unajenga pia diplomasia ya kiuchumi,” amesema.

Kwa upande wake, Balozi wa China nchini Tanzania Chen Mingjian amesema kujifunza lugha hiyo na kusoma nchini China kunazidi kuwa maarufu kwa Watanzania.

“Shindano hili linaweza kutoa maarifa zaidi na mambo mapya kuhusu mbinu za kufundishia, kuboresha ustadi wa kufundisha kupitia jukwaa hili na kutangaza kwa ustadi uzuri wa lugha ya Kichina kwa wanafunzi wa Kitanzania,” amesema/

Makamu Mkuu chuoni hapo, Profesa William Anangisye amesema kuwa taasisi ya kichina chuoni hapo ilianzishwa chini ya makubaliano kati ya Chuo Kikuu na makao makuu yaliyoko Hanban na Chuo Kikuu cha Kawaida cha Zhejian nchini China ili kuwezesha lugha ya Kichina.

Profesa Anangisye amesema taasisi hiyo inalenga kukidhi haja ya Tanzania ya kuelewa utamaduni, teknolojia na ujuzi wa lugha ya Kichina na kuongeza maelewano kati ya watu wa China na Tanzania.

Vile vile amesema taasisi hiyo imekuwa ikifanya kazi kama jukwaa la mabadilishano ya kijamii, kisiasa na kiuchumi baina ya nchi hizo mbili.

Amesema taasisi hiyo imewaunganisha wanafunzi wa vyuo vikuu na makampuni nchini Tanzania kabla ya kuhitimu elimu yao.

Amesema wafanyakazi wa Taasisi hiyo wamekuwa wakifanya kazi kwa bidii kuhakikisha kuwa vijana wa Kitanzania wanajifunza lugha ya Kichina ili kuboresha uwezo wao wa kiushindani katika kukuza taaluma na kujiendeleza pia.

“Juhudi zetu za pamoja zimewawezesha wanafunzi wetu na kitivo, kupanua mtandao wetu wa kimataifa na kuimarisha sifa yetu ndani na nje ya Tanzania,”amesema.

Awali, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Zhang Xiaozhen amesema mashindano hayo yalishirikisha walimu 54 wa China kutoka nchi 11. Kutoka Tanzania, Zambia, Rwanda, Msumbiji, Mali, Madagascar, Liberia, Kenya, Ghana, Misri na Cameroon.

Amewahimiza walimu zaidi wa China kushiriki katika shindano hilo ili kuongeza dhana za kitaaluma, ujuzi wa maarifa na utendaji wa walimu wa ndani wa China barani Afrika.

You Might Also Like

Chukueni Mkopo, Kwenye Taasisi Zilizopewa Leseni Na BOT

Watumishi wa serikali watakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Tanzania Yapokea Faru 18 Kutoka Afrika Kusini

Mwongozo wa Mafunzo Elekezi Kwa Walimu Wapya Kazini Mbioni Kukamilika

Mnyororo wa Biashara Kariakoo Unafanywa Na Wageni

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kumekucha Uzinduzi wa Washirika wa Tamasha, Tuzo Za Filamu Tanzania 2025
Next Article Majaliwa Awaagiza Wahandisi Kuzingatia Miiko, Maadili  Ya Taaluma Yao
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tanzania Na Namibia Kuongeza Juhudi Kukuza Ushirikiano Wa Kiuchumi
Habari May 21, 2025
Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe
Habari May 21, 2025
TDB Yaheshimisha Tasnia Ya Maziwa
Habari May 21, 2025
Dkt. Ndumbaro : Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Imefanikiwa 
Habari May 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?