MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: KINABO: NICHAGUENI NILETE MAJI, BARABARA KIBAMBA
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > KINABO: NICHAGUENI NILETE MAJI, BARABARA KIBAMBA
Habari

KINABO: NICHAGUENI NILETE MAJI, BARABARA KIBAMBA

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Mwandishi Wetu

DAR ES SALAAM: MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Kibamba kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Edward Kinabo, amewataka wananchi wa jimbo hilo kumchagua ili aweze kutatua tatizo la muda mrefu la maji.

Akizungumza katika Kata ya Saranga, Kinabo amesema serikali ya CCM imeshindwa kutatua changamoto hiyo na haina mpango wa kufanya hivyo. “Wanakibamba nichagueni muhanga mwenzenu, msimchague mkazi wa Oysterbay, maana hamtatoboa,” amesema.

Habari Picha 9783

Kinabo ameeleza kuwa ameamua kugombea kwa sababu anaifahamu vizuri kero ya maji akiwa mkazi wa Goba, anayenunua maji ya madumu kama wakazi wengine wa Kibamba.

Amesisitiza kuwa barabara ya Morogoro inayopitisha makontena ya biashara kubwa haijawanufaisha wakazi wa Kibamba kwani hakuna barabara za lami wala huduma za msingi kama maji.

“Nimegombea Kibamba ili kumaliza shida ya maji. Jimbo hili ndilo la kwanza kutoka mkoa wa Pwani lilipo chanzo cha maji cha Ruvu, lakini maji yanaelekezwa Oysterbay badala ya Kibamba,” amesema.

Amewaomba wananchi kuipiga chini CCM na kuichagua CHAUMMA, akisisitiza kuwa ana uzoefu wa kuandaa miswada na kuuliza maswali bungeni. “Nitumeni nikasukume maji,” ameeleza.

Habari Picha 9782

Pia amemwomba mgombea urais wa chama chake kuhakikisha anatenga ruzuku kwa ajili ya miundombinu ya maji, akibainisha kuwa licha ya ushuru wa shilingi 100 kwa kila lita ya mafuta kutozwa kwa ajili ya miundombinu, bado Kibamba haina barabara zinazopitika.

“Nagombea jimbo hili ili tukarabati barabara za mitaani, hususani Kibamba, kama ilivyo Mwananyamara na Kinondoni ambapo angalau zipo za kupakazia,” amesema.

Kinabo amedai kuwa Halmashauri ya Ubungo inakusanya jumla ya shilingi bilioni 131 kwa mwezi kwa ajili ya maendeleo, lakini wananchi wa Kibamba hawajanufaika nazo. Aliongeza kuwa sera ya ubwabwa siyo masihara, kwani shule bado zinachangia chakula na madawati, licha ya mapato ya madini.

“Nataka serikali ya CHAUMMA iongeze ruzuku kutoka sh. 10,000 hadi 30,000,” amesisitiza.

Akizungumzia mgombea wa CCM, Anjela Kairuki, Kinabo alihoji ufanisi wake, akidai kuwa mtangulizi wake, Issa Mtemvu, alishindwa kuwaletea maendeleo. “Kama Kairuki amekuwa Waziri wa TAMISEMI, jiulizeni ametufanyia nini wakazi wa Kibamba?,” amesema.

You Might Also Like

Mabasi  Mapya Ya Mwendokasi Yaanza Kazi Njia Ya  Kimara, Gerezani na Kivukoni

Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa

AUWSA Kutibu Maji Taka Yatumike Kwenye Kilimo

Erio atoa elimu ya bidhaa bandia kwenye mabanda nanenane

Rais Samia Azungumzia Mafanikio Ya Nishati Nchini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TTCL Yawahakikishia Wateja  Miundombinu Yenye Kuboresha Maisha Yao
Next Article Samia Aendeleza Kampeni Mwanza, Azungumza na Wananchi Misungwi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?