MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kikwete Awahimiza Wahitimu wa UDSM Kuwa Mabalozi Wazuri wa Chuo 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Uncategorized > Kikwete Awahimiza Wahitimu wa UDSM Kuwa Mabalozi Wazuri wa Chuo 
Uncategorized

Kikwete Awahimiza Wahitimu wa UDSM Kuwa Mabalozi Wazuri wa Chuo 

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, amewaasa wahitimu kuwa mabalozi wazuri wa chuo hicho ambacho amelitaja kuwa bora kuliko vyuo vyote nchini.
Kikwete aliwaasa hayo baada ya kuhitimishwa kwa Mahafali ya 55, duru ya nne, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Habari Picha 10475
“Tunawapongeza na kuwatakia kila la heri katika shughuli mbalimbali. Pia endeleeni kuwa mabalozi wazuri wa chuo hiki, ambacho ni cha kwanza kuanzishwa na kinaendelea kuwa cha kwanza katika masomo,” amesema Kikwete.
Naye Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa William Anangisye, amesema chuo kinaendelea na kazi ya mapitio, uhakiki, uidhinishaji na maombi ya ithibati ya mitaala ya programu mbalimbali.
Amesema zaidi ya mitaala 250 imepitiwa na inatarajiwa kuwasilishwa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kwa ajili ya kupitishwa, ambapo takribani mitaala 242 ya ngazi ya shahada ya awali na uzamili tayari imewasilishwa.
“Hadi sasa, mitaala 49 imepata ithibati kwa mwaka 2025/26. Miongoni mwa programu mpya zilizopata ithibati ni shahada ya awali ya sayansi katika fizikia, na shahada ya umahiri ya fizikia ya tiba.
Habari Picha 10476
“Kutunuku shahada na stashahada mwaka 2025, wanataaluma 92 ambao Mlimani 68, MUCE 18, DUCE 6, walipanda madaraja kutoka wahadhiri kuwa wahadhiri waandamizi, kutoka wahadhiri waandamizi kuwa Profesa Washiriki, na kutoka Profesa Washiriki kuwa Profesa,” amesema.
Profesa Anangisye ameongeza kuwa katika duru hiyo ya nne ya Mahafali ya 55, wahitimu 2,046 wamehudhurishwa, wakiwemo: shahada za uzamivu 65,  za umahiri 522, za uzamili 26, za awali 1,291, stashahada 126 na astashahada 16.
Ameasa wahitimu kutumia elimu waliyopata kuleta faida kwa Watanzania, akisisitiza kwamba chuo kina jukumu la kuhakikisha masomo yanayofundishwa yanaendana na mahitaji ya soko ili kupunguza changamoto za ajira na kuwapa wanafunzi uwezo wa kujiajiri mara wanapohitimu.
Habari Picha 10477
Profesa huyo pia amesema, endapo ajira za serikalini au kutoka sekta binafsi zitachelewa kupatikana, wahitimu wawe wepesi kuangalia sehemu nyingine ambapo maarifa na ujuzi wao unaweza kutumika kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Balozi Mwanaidi Maajar, amepongeza wahitimu hao akisema ni siku yao ya mwisho ya safari yao kitaaluma, bali ni mwanzo wa safari mpya iliyojaa fursa, majukumu na nafasi ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii na ulimwengu kwa ujumla.
Habari Picha 10478
Habari Picha 10479
Habari Picha 10480
Habari Picha 10481

You Might Also Like

Profesa Kabudi Amimina Pongezi TEA

Bandari ya Kilwa kuleta mapinduzi sekta ya uvuvi nchini

GWSON yawakumbuka watoto wenye vichwa vikubwa,mgongo wazi kumbukizi ya Mwl.Nyerere

Waziri Jenista akabidhiwa ofisi rasmi na Ummy Mwalimu

Samia Kalamu Award yasogeza Mbele

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ufanisi Wa TANESCO Katika  Utekelezaji Na Usimamizi Wa Miradi Umeleta Mfumo Madhubuti Wa Nishati- Ndejembi
Next Article Petroli Yaendelea Kushuka Bei Desemba
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Msama Aipongeza Hotuba Ya Samia, Atoa Neno Kwa Vijana, Wazee, Wanaharakati
Habari December 4, 2025
Profesa Silayo Aaga, Jawara Kuchukua Uongozi Mpya wa AFWC25
Habari December 3, 2025
Mpango Wa Taifa Wa Teknolojia Uko Mbioni Kuja-Serikali
Habari December 3, 2025
Petroli Yaendelea Kushuka Bei Desemba
Habari December 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?