MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Atoa Rai Kuhusu Afya ya Akili kwa Vijana
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Atoa Rai Kuhusu Afya ya Akili kwa Vijana
Habari

Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Atoa Rai Kuhusu Afya ya Akili kwa Vijana

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi 
MBEYA: KATIBU Mkuu Kiongozi wa Zanzibar, Zena Ahmed Said, amezitaka taasisi za dini pamoja na  vyuo vikuu, kuhakikisha zinakuwa na wataalamu wa ushauri nasaha kwa ajili ya kuwasaidia vijana wanaokumbwa na msongo wa mawazo.
Akizungumza wakati wa kufunga Kongamano la Kitaifa la Vijana lililofanyika mkoani Mbeya, Zena amesisitiza kuwa afya ya akili kwa vijana imeendelea kuwa changamoto kubwa, jambo linalohitaji juhudi za pamoja kutoka kwa jamii, taasisi za elimu, na viongozi wa dini.
“Vijana wanapokumbwa na changamoto za kisaikolojia, ni muhimu wawe na sehemu salama ya kupata ushauri. Vyuo na taasisi za dini zina nafasi kubwa ya kujenga kizazi chenye mtazamo chanya wa maisha,” amesema.
Ameeleza kuwa baadhi ya vijana wamekuwa wakijihusisha na matumizi ya dawa za kulevya, bangi, gundi, na hata dawa za usingizi za hospitali, kutokana na msongo wa mawazo na ukosefu wa mwelekeo.
Katika kongamano hilo, amewaonya vijana dhidi ya kujilinganisha na wengine kupitia mitandao ya kijamii, akisema hali hiyo inachochea hisia za matamanio na kusababisha msongo wa mawazo.
“Mitandao ya kijamii haioneshi uhalisia wa maisha ya watu. Wengine wanaopost nyumba au magari si yao, lakini ukianza kujilinganisha nao, unajikuta unaathirika kisaikolojia,” amesema.
Zena pia amewashauri vijana kuwa makini na kila uamuzi wanaoufanya, kwani kila hatua waliyochukua ina athari nzuri au mbaya  kwa maisha yao ya sasa na ya baadaye.
Aidha, aliwataka vijana kujiepusha na tabia ya kufuatilia taarifa mbaya mtandaoni au kwenye vyombo vya habari, kama vile migogoro na vita vya kimataifa, kwani huongeza mzigo wa kiakili na kuchochea wasiwasi usio wa lazima.
“Kuna watu ambao kila siku wanafuatilia taarifa mbaya vita, majanga, au migogoro hali hii huwajaza hofu na kuwafanya waishi kwa msongo. Jifunze kuchuja taarifa unazozipokea,” amesema.
Kongamano hilo la vijana lilikutanisha washiriki kutoka maeneo mbalimbali ya nchi kwa lengo la kujadili changamoto na fursa zinazowakabili vijana katika dunia ya sasa, ikiwemo suala la afya ya akili, mitandao ya kijamii, ajira na maadili.

You Might Also Like

Serikali Kupeleka Umeme Maeneo Ya Kimkakati

Kabonaki: Jiungeni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Hiari

Tanzania yqpata dola bilioni 2.3 kwa kuuza matunda, kunde nje

Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki

Kifo cha Ndugai Kisigeuzwe Siasa – Familia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wagonjwa 472 Waonwa Na Daktari Wa Mifupa MOI, 40 Wapendekezwa Kufika Dar kwa Matibabu
Next Article VETA Yajipanga Kutoa Mafunzo Yanayoendana na Teknolojia ya Kisasa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
Serikali Yapeleka Sh Bil 10 Kwa Kiwanda Cha Viuadudu Cha TBPL
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?