MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Katambi Aitaka NDC Kuleta Mapinduzi Makubwa Ya Viwanda
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Katambi Aitaka NDC Kuleta Mapinduzi Makubwa Ya Viwanda
Habari

Katambi Aitaka NDC Kuleta Mapinduzi Makubwa Ya Viwanda

Author
By Author
Share
3 Min Read

 

Na Lucy Lyatuu

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Patrobas Katambi, ameliagiza Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) kuhakikisha inaleta mapinduzi makubwa ya viwanda kwa kufungua viwanda vingi na kutengeneza fursa nyingi hususani kwa vijana.

Aidha amelitaka kuongeza kasi na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yake ili kuunga mkono juhudi za Serikali za kuimarisha sekta ya viwanda.

Katambi ametoa kauli hiyo  alipofanya ziara ya kikazi katika makao ya shirika hilo, ambapo alisisitiza umuhimu wa NDC kusimamia kwa umakini maeneo yote yaliyo chini ya dhamana yake lakini kufanya kazi kwa kasi kubwa na yenye weledi.

Amesema Serikali imejipanga kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika viwanda, ikiwemo kuwezesha upatikanaji wa mitaji na ushauri wa kibiashara, kwa lengo la kupanua wigo wa ajira hasa kwa vijana.

Habari Picha 10596

Amefafanua kuwa mpango wa Serikali ni kuleta mageuzi makubwa ya viwanda kuanzia vidogo, vya kati hadi vikubwa, ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa taifa.

“NDC ilenge  kuwa na viwanda vidogo sana, vidogo vya kati, n ahata vikubwa huku ikihakikisha kuwa viwanda vilivyodorora vinafufuliwa kwa haraka ikiwa ni tija ya kuongeza viwanda zaidi,” amesema.

Aidha, amehimiza mshikamano, mashauriano ya mara kwa mara na kuondoa urasimu usio wa lazima ndani ya shirika, akisisitiza kuwa NDC inapaswa kuwa kiungo kati ya Serikali na wananchi badala ya kuwa kikwazo.

Ameongeza kuwa mafanikio ya kiuchumi ya nchi yoyote yanategemea uwepo wa viwanda imara vinavyoweza kuzalisha ajira na kuongeza thamani ya rasilimali zake.

Awali akizungumza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NDC, Valentine Simkoko, amesema shirika hilo linasimamia  miradi  mbalimbali ya kimkakati na  linaendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi.

Aliitaja baadhi ya miradi inayosimamiwa na NDC kuwa ni Pamoja na Mchuchuma na Liganga, Magadi Soda ya Engareka, pamoja na tathmini ya mali za wananchi wanaohusika katika miradi ya makaa ya mawe Katewaka na chuma ghafi cha Maganga Matitu.

Simkoko ameongeza  NDC pia imeingia mikataba ya ubia na wawekezaji katika mradi wa chuma wa Maganga Matitu, pamoja na kusaini mkataba na kampuni ya Labiofam S.A. kwa ajili ya kuhamisha teknolojia ya uzalishaji wa mbolea hai nchini.

 

You Might Also Like

Miaka 60 Mikumi na mapinduzi makubwa sekta ya utalii

Rais Mwinyi Ajionea Mifumo Mbalimbali Banda La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba

Miaka Minne Ya Samia Na Sekta Ya Elimu

Nchi Za SADC Zahimizwa Kutunza, Kulinda Amani

TARI Mlingano Yaleta Mapinduzi ya Mkonge, Viungo na Sayansi ya Udongo Tanzania

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waziri Sangu Aagiza Hatua Kali kwa Waajiri Wanaokwepa Kuwasilisha Michango NSSF
Next Article Mchengerwa Aongoza Ujumbe Wa Tanzania Kwenye Uzinduzi Wa Mkutano Wa Dunia Wa Tiba Asili
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?