MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari

Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Palamagamba Kabudi, amesema kutosoma vitabu kunaweza kufanya ubongo kusinyaa na kupunguza uwezo wa kufikiri.
Kabudi amesema maelezo hayo ni kwa mujibu wa wataalam wa afya ya akili.
Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya 32 ya Kimataifa ya Vitabu Tanzania yanayoendelea Dar es Salaam.
Habari Picha 10413
“Vitabu ni tiba,  husadia kuongeza maarifa, kuboresha fikra, kuimarisha msamiati na ufasaha wa lugha, kuongeza ubunifu, kupunguza msongo wa mawazo na kukuza nidhamu,” amesema.
Ametoa wito wa kujengea watoto utamaduni wa kusoma vitabu na kuhimiza ubunifu katika uchapishaji.
Kabudi amesema maktaba ni taasisi muhimu kwa taifa lolote linalojitambua, hivyo kuna haja ya kuimarisha uhusiano kati ya maktaba na waandishi wa vitabu ili kuendeleza maktaba za taifa.
Pia amewataka wadau wa lugha ya Kiswahili kutumia majukwaa yaliyopo kuboresha mchango wao katika kutunza uchumi na tamaduni.
Amesema sekta ya vitabu ni chanzo cha ajira na kipato kupitia uandishi, uchapishaji na uuzaji wa vitabu.
Habari Picha 10411
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba, Dkt. Mboni Ruzegea, amesema maadhimisho hayo yamelenga kukumbushana umuhimu wa vitabu nchini.
Amesema vitabu vinachangia kujenga ujirani mwema, diplomasia na uchumi.
Pia ameitaka serikali kuendelea kuipa nguvu sekta ya vitabu kwa kuwa bila vitabu na maktaba imara, haiwezekani kujenga uchumi na maarifa.
Habari Picha 10412
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wachapishaji wa Vitabu (PATA), Hermes Damian, amemwomba Waziri Kabudi kuwasaidia katika kuimarisha sekta ya vitabu na kuwezesha utungaji wa sera madhubuti ya uandishi na usomaji wa vitabu.
Amesema sera hiyo itasaidia kujenga taifa linalovithamini vitabu na kutoa mchango wa kifikra, maarifa na weledi katika nyanja mbalimbali za maisha na maendeleo.
Pia ameeleza kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza utegemezi wa taarifa zilizotafuniwa tayari.
Habari Picha 10399
Habari Picha 10400

You Might Also Like

Wafanyakazi Wa Majumbani  700 Wapatiwa Mafunzo VETA

Wadau Wakaribishwa Kuwekeza Katika Uchakataji, Biashara ya Mkonge Nchini

Fursa za Uwekezaji Kanda ya Ziwa: Buzwagi na Maeneo Mengine ya Kimkakati

Tume Ya Mipango Yaelekeza Waandishi Wa Habari Kutoa Elimu Ya Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050

Dkt. Tumbo Aitaka Jamii Kuelimishwa Namna Bora Ya Kuhifadhi Taka

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Next Article Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?