MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: JOWUTA,IFJ na THRDC kutoa mafunzo ya kuripoti uchaguzi mkuu.
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > JOWUTA,IFJ na THRDC kutoa mafunzo ya kuripoti uchaguzi mkuu.
Habari

JOWUTA,IFJ na THRDC kutoa mafunzo ya kuripoti uchaguzi mkuu.

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: CHAMA cha Wafanyakazi Katika Vyombo vya Habari nchini(JOWUTA) kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la Waandishi Duniani(IFJ) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binaadamu(THRDC) wanatarajia kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini jinsi ya kuripoti uchaguzi mkuu wakiwa salama.
Mafunzo hayo ambayo yanaratibiwa na JOWUTA katika awamu ya kwanza yanatarajiwa kufanyika Aprili 2025 katika Kanda tatu nchini, ambazo ni Pwani , Nyanda za Juu Kusini na Kaskazini ambayo itaandamana na maadhimisho ya siku ya kimataifa ya uhuru wa habari ambayo itafanyika jijini Arusha.
Mwenyekiti wa JOWUTA Taifa, Mussa Juma amesema hayo katika taarifa aliyoitoa baada ya viongozi wa JOWUTA kutembelea Makao Makuu ya THRDC jijini Dar es salaam, kufanya mazungumzo na Mratibu wa kutaifa wa mtandao huo, Onesmo Ole Ngurumwa.
Juma amesema katika mkutano wa waandishi wa habari Afrika uliofanyika nchini Senegal na baadae Rwanda, JOWUTA imeomba IFJ na Shirikisho la Waandishi Afrika(FAJ) kusaidia mafunzo kwa wanahabari Tanzania ili waweze kuripoti uchaguzi kwa haki na salama.
“Niliomba watusaidie mafunzo na baada ya majadiliano baina yao IFJ ikakubali kugharamia sehemu ya mafunzo,” amesema.
Amesema kutokana na mafunzo kuhitaji gharama kubwa JOWUTA iliamua kuanza kutafuta wadau wengine kushirikiana nao wakiwepo THRDC.
Naye Mratibu wa THRDC Ngurumwa amesema THRDC itachangia sehemu ya gharama za kufanikisha mafunzo kwa wanahabari nchini.
“Sisi kama wadau wakubwa wa watetezi wa haki za binadamu wakiwepo waandishi wa habari tutachangia mafunzo haya ili waandishi waweze kuripoti vyema uchaguzi mkuu kwa haki,bila upendeleo lakini wakibaki salama,” amesema.
Amesema THRDC kwa muda sasa imekuwa ikitoa mafunzo mbalimbali kwa waandishi ikiwepo sheria za uchaguzi lakini pia mafunzo ya ulinzi na usalama kazini.
Awali Katibu Mkuu wa JOWUTA, Seleman Msuya amesema JOWUTA ndio chama pekee kinachotambulika kisheria nchini ambacho kinatetea maslahi ya wafanyakazi katika vyombo vya habari na masuala ya mazingira bora ya kazi zao.
Amesema THRDC kukubali kufanya kazi na JOWUTA hawajakosea na watakuwa pia wametimiza wajibu wao kuwasaidia watetezi wa haki za binadamu kufanyakazi katika mazingira salama.
Hata hivyo alitoa wito kwa wadau wengine kusaidia wanahabari kupitia JOWUTA ambayo ina zaidi ya wanachama 400 nchi nzima.

You Might Also Like

Utafiti UDOM Wawezesha Plastiki Kutengeneza Mafuta Mazito Ya Viwanda, Mkaa Na Tiles

Rais Samia kufungua kikao kazi cha watendaji serikalini

Wakulima Waomba Watafiti Wa  AGRISPAK, Kuwatafutia Mbinu Kukabili Nzi Weupe

TEA Kukarabati Jengo La Bodi Ya Maktaba Kwa Milioni 300

VETA Yatembelea Kiwanda Cha Kutengeneza Nyumba Bila Kutumia Tofali

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Chalamila: Serikali Imewekeza Kupatikana Wataalamu Wa Usingizi, Yapunguza Vifo Vinavyotokana Na Upasuaji
Next Article Wenye Ulemavu Wa Ngozi Wakumbukwa Kupitia FDH, Wapewa Msaada Wa Milioni 20
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mara Yapaa: Miaka Minne Ya Mafanikio Chini Ya Rais Samia
Habari July 18, 2025
Serikali Yazindua Mafunzo Ya Mtandao Ya Afya Moja
Habari July 16, 2025
Watu Zaidi Ya 3500 Wapatiwa Huduma Ya Kisheria Wizara Ya Katiba Na Sheria
Habari July 16, 2025
Ubunifu Na Kufanya Tafiti Kwawezesha UDOM Kupokea Tuzo
Habari July 16, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?