MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: JAB Yasisitiza Ithibati Kama Njia ya Kuimarisha Ubora na Uaminifu wa Habari
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > JAB Yasisitiza Ithibati Kama Njia ya Kuimarisha Ubora na Uaminifu wa Habari
Habari

JAB Yasisitiza Ithibati Kama Njia ya Kuimarisha Ubora na Uaminifu wa Habari

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imesisitiza kuwa utekelezaji wa mfumo wa ithibati kwa waandishi na watangazaji wa habari ni mkakati muhimu wa kukuza uaminifu, weledi na ushindani wa sekta ya habari katika uchumi wa kisasa unaotegemea taarifa sahihi na za kuaminika.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Patrick Kipangula, ameeleza hayo alipozungumza katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji (ABC) uliofanyika Februari 13, 2026 jijini Dodoma,
Alisema mfumo huo unalenga kuimarisha taaluma kwa kuzingatia misingi ya kitaaluma, maadili na uwajibikaji kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229.
Habari Picha 11234
Alifafanua kuwa ithibati si chombo cha kudhibiti maudhui ya habari, bali ni utaratibu wa kuweka viwango vinavyolinda hadhi ya taaluma na kuongeza imani ya umma kwa vyombo vya habari.
Aliongeza kuwa katika mazingira ya ushindani wa kidijitali, uaminifu wa chanzo cha habari ndiyo rasilimali kuu ya chombo cha habari.
Aidha, alieleza kuwa vyombo vinavyowekeza katika kuimarisha weledi wa watumishi wake hujiongezea nafasi ya kuvutia wawekezaji, matangazo na ushirikiano wa kimataifa, kutokana na kuongezeka kwa thamani ya ubora na uwajibikaji katika soko la habari.
Kwa mujibu wa wadau walioshiriki mkutano huo ulioandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ushirikiano kati ya msimamizi wa maudhui na wadau wa tasnia ni msingi muhimu wa kujenga sekta imara inayochangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Uimarishaji wa mfumo wa ithibati umeelezwa kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kukuza taaluma za ubunifu na mawasiliano kwa viwango vinavyokidhi mahitaji ya ndani na kimataifa, huku sekta ya habari ikiendelea kuwa nguzo ya uwazi, uwajibikaji na maendeleo endelevu.
Takwimu zinaonesha kuwa zaidi ya waandishi 3,200 kati ya 3,900 walioomba vitambulisho vya uandishi wa habari (Press Card) wamekidhi vigezo vya kisheria na kuthibitishwa, jambo linaloashiria mwitikio chanya na dhamira ya sekta kujiimarisha kitaaluma.

You Might Also Like

Mawaziri Tanzania Profesa Mkenda, Silaa Mkutanoni Rwanda

TMDA Kudhibiti Bidhaa Za Tumbaku Ili Wananchi Wasiendelee Kupata Madhara

Wananchi Wahimizwa Kulinda Maeneo Yaliyohifadhiwa  Kisheria- Kamishna  Wakulyamba

TEITI Yashiriki Maonesho ya Nane ya Uwekezaji Sekta ya Madini Geita

Changamoto ya uelewa mwiba kwa wasafirishaji Comoro

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mwelekeo Mpya wa Viwanda: Safari ya Siku 100 za Mageuzi ya Kiuchumi
Next Article Makamu wa Rais Asisitiza Ubunifu, Uwekezaji Soko La Hisa La Dar es Salaam
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Makamu wa Rais Asisitiza Ubunifu, Uwekezaji Soko La Hisa La Dar es Salaam
Habari February 13, 2026
Mwelekeo Mpya wa Viwanda: Safari ya Siku 100 za Mageuzi ya Kiuchumi
Makala February 13, 2026
Watu Wenye Ulemavu Nchini Wafikia Mil 5.3
Habari February 12, 2026
MAIPAC Yasisitiza Maadili Na Usalama Kwa Waandishi Wa Habari
Habari February 12, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?