MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Hazina yaanza kuwalipa wanachama 465 wa TALGWU
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Hazina yaanza kuwalipa wanachama 465 wa TALGWU
Habari

Hazina yaanza kuwalipa wanachama 465 wa TALGWU

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: SERIKALI imeanza kuwalipa wafanyakazi 465 kati ya 645 wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania ( TALGWU), kupitia mfuko mkuu wa serikali – Hazina.
Katibu Mkuu wa TALGWU, Rashid Mtima amesema hayo alipozungumza na waandishi wa Habari mkoani Dar es Salaam, na kuongeza kuwa wafanyakazi hao wameanza kulipwa Julai mwaka huu.
Mtima amesema kundi hilo la wafanyakazi awali lililipwa mishahara yao kupitia mapato ya halmashauri.
Amesema TALGWU katika vikao na majadiliano mbalimbali na serikali mara kadhaa ilikuwa ikizungumzia changamoto, kero na kadhia wanazopitia watumishi hao ambao ni wanachama wao.
Amesema watumishi hao wakati wakilipwa na halmashauri, walipitia changamoto za kutolipwa mishahara kwa wakati, kukosa huduma ya matibabu kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kutokana na makato kutowasilishwa kwa wakati.
Vile vile kutokukopesheka katika baadhi ya taasisi za fedha ikiwa ni pamoja na kupata usumbufu mkubwa pindi wanapostaafu kutokana na makato ya michango yao kutokuwasilishwa kwa wakati katika mfuko wa hifadhi ya jamii.
“Hii ni hatua kubwa sana iliyochukuliwa na serikali kwani itaondoa kero za muda mrefu, itaongeza ari na morali ya kufanya kazi.
“Pamoja na pongezi hii tunaiomba tena serikali kuangalia upya na kufanya mchakato ili wanachama wetu 180 waliosalia katika majiji na manispaa ambao bado wanalipwa kwa mapato ya ndani ya halmashauri nao waanze kulipwa kupitia hazina ” amesema.

You Might Also Like

TUCTA: Wafanyakazi Jitokezeni  Kwa Wingi Kwenda Kupiga Kura Mchague Viongozi Watakaolinda  Maslahi Yenu  

PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari

TEITI Yashiriki Maonesho ya Nane ya Uwekezaji Sekta ya Madini Geita

JKCI Imeona Wagonjwa Zaidi ya Laki Saba Kwa Miaka Minne

Asilimia 22 Ya Vijana Wanakumbwa Magonjwa Yasiyo Ya Kuambukizwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mpango wa Shule Salama Unaongeza ulinzi Kwa Watoto
Next Article China Yafundisha Wanafunzi DIT kuzifikia fursa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?