MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: DC Atoa Wito kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Kuzingatia Sheria Ndogondogo za Halmashauri
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > DC Atoa Wito kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Kuzingatia Sheria Ndogondogo za Halmashauri
Habari

DC Atoa Wito kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Kuzingatia Sheria Ndogondogo za Halmashauri

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MKUU wa Wilaya ya Kongwa ametoa wito kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) kufuatilia na kuzingatia sheria ndogondogo zinazopitishwa katika halmashauri na vijiji, akisema zinaweza kuwa na mchango mkubwa katika mabadiliko ya sheria kuu za kitaifa.
Amesema hayo alipotembelea banda la LRCT, katika Maonesho ya Nanenane ya Kitaifa yanayoendelea mkoani Dodoma,
Amesema sheria hizo, ingawa zinaweza kuonekana ndogo au za kawaida, ndizo zinazogusa maisha ya wananchi moja kwa moja na mara nyingine zinatatua kero kubwa ambazo hazijawekewa sheria katika ngazi ya kitaifa.
“Inawezekana jambo linaonekana ni la kawaida lakini kule chini kwenye jamii linakuwa ndiyo kero kubwa ya wananchi. Halmashauri nyingine hujiwekea sheria ndogondogo ambazo zinafanya vizuri, lakini halmashauri nyingine hazijui kama kuna mahali panafanyika hivyo,” amesema.
Amesisitiza kuwa sheria hizo ndogondogo zinaweza kuchangia katika uundaji wa sheria mama kwa sababu zinatokana na hali halisi ya jamii. Na kutoa mfano wa sheria za mazingira zinazotungwa katika vijiji vya Wilaya ya Kongwa ambazo, kwa mujibu wake, zinaweza kuwa mfano bora kwa halmashauri nyingine nchini.
Naye Wakili kutoka katika tume hiyo, Vick Mbunde amesema kuwa tume hiyo ilianzishwa mwaka 1981 na kuanza kazi rasmi mwaka 1983, ikiwa na jukumu la kufanya mapitio na marekebisho ya sheria mbalimbali nchini.
Amesema licha ya changamoto ya bajeti, tume imefanikiwa kufanya mapitio ya sheria nyingi, zikiwemo:
Sheria ya uchaguzi, Sheria ya mtoto, kufuatia kuongezeka kwa ukatili dhidi ya watoto, Sheria ya vinasaba (DNA), baada ya kutokea mgawanyiko mkubwa wa maoni na Sheria zinazohusu sekta ya kilimo,
Mbunde alibainisha kuwa mchakato wa marekebisho ya sheria hufanywa kwa kuangalia mfumo mzima unaohusiana na eneo husika. Kwa mfano, katika sekta ya kilimo, tume huchambua sheria zote zinazogusa sekta hiyo kwa pamoja.
Hata hivyo, amekiri kuwa tume hukumbwa na changamoto ya ufinyu wa bajeti, hali nayosababisha kufanya mapitio ya sheria chache tu kwa mwaka.
“Kwa mwaka tunaweza kufanya mapitio ya sheria 10 hadi 12, lakini tunazo zaidi ya 400. Kwa mujibu wa utaratibu, sheria inapaswa kufanyiwa tathmini kila baada ya miaka mitano. Kwa hiyo tuko taratibu sana kwa sababu ya bajeti,” amesema,
Pia amesema changamoto nyingine ni uelewa mdogo wa wananchi kuhusu umuhimu wa kushiriki katika kutoa maoni wakati wa mapitio ya sheria. Alisema wengi hujitokeza kutoa maoni tu endapo suala linawagusa moja kwa moja.
Tume hiyo inaendelea kutumia mbinu mbalimbali kuongeza ushiriki wa wananchi, ikiwemo kupeleka timu katika maeneo ya jamii ili kupata maoni ya moja kwa moja.

You Might Also Like

Vyama Vya Wafanyakazi Kujadili Hatma Ya Wafanyakazi TAZARA

Dkt Biteko Awasili Nchini India Kwa Ziara Ya Kikazi

TMA yawafikia taasisi za utafiti wa kilimo

Majaliwa Awaagiza Wahandisi Kuzingatia Miiko, Maadili  Ya Taaluma Yao

VETA Kihonda Waja Na Mashine Ya Kusaga Chumvi Sabasaba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TPHPA Yaleta Mapinduzi Mapya Katika Kilimo Kupitia Teknolojia ya Vinasaba
Next Article Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mtego wa Inzi Wa Matunda Suluhisho Salama kwa Wakulima
Habari August 7, 2025
Mafua, Kifua Yadaiwa Kusababisha Kifo cha Job Ndugai
Habari August 7, 2025
Zimbabwe Yakabidhi Uenyekiti Kwa Madagascar
Habari August 7, 2025
Tume ya Kurekebisha Sheria Yatoa Onyo Kali kwa Wanaovunja Sheria za Umwagiliaji
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?