MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Chukueni Mkopo, Kwenye Taasisi Zilizopewa Leseni Na BOT
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Chukueni Mkopo, Kwenye Taasisi Zilizopewa Leseni Na BOT
Habari

Chukueni Mkopo, Kwenye Taasisi Zilizopewa Leseni Na BOT

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
BENKI Kuu Ya Tanzania (BOT)
 imesema watu wengi wanaendelea kuumia kwa kukosa uelewa wa kujua kinachotakiwa, haki zao muhimu na wajibu wao wakati wanapotaka  mkopo.
Ofisa Mkuu Mwandamizi kutoka Idara ya Usimamizi wa Huduma Ndogo za Fedha kutoka BOT, Deogracious Manyama amesema hayo Dar es Salaam wakati benki hiyo ikiendelea na kampeni   ya kuelimisha watanzania kuhusu hatua zinazotakiwa wakati wa kukopa fedha.
Amesema BOT inafanya kampeni kwa sababu  licha ya kuwepo kanuni bora, sheria na sera za fedha bado wanaendela  kuumia.
” Tumefanya utafiti na kubaini kuwa kinachosababisha kuendelea kuumia ni kwa kukosa uelewa wa kujua vitu  gani vya muhimu, haki wakati wanapokwenda kuchukua mkopo” amesema na kuongeza  kuwa  maumivu hayo hukutana nao wanapokutana na watoa huduma ambao sio waaminifu.
Amesema umekuwepo ushahidi kwamba watanzania wamekuwa wakinyanyasika, kudhulumiwa na kupata hasara nyingi kwenye eneo la mikopo.
” Hivyo BOT imeona hiyo changamoto itatuliwe kwa kutoa elimu kwa umma ambapo wanapita mtaa kwa mtaa kwa mkoa wa Dar es Salaam ili kutoa elimu, ” Amesema na kuongeza kuwa mpaka sasa wameshapitia eneo la Kigamboni, Temeke na Ilala.
Amesema kwa sasa wanaelekea eneo la Kinondoni na Ubungo na kampeni hiyo inapita mtaa kwa mtaa, kitongoji kwa kitongoji lengo likiwa kuelimisha  watanzania ili wanapokwenda kukopa wawe na vitu muhimu vya kuzingatia.
Amesema kampeni imekuja ili kuwafikia wananchi wakiwa kwenye maeneo yao ya kazi  na kwa siku wanauwezo wa kufikia watu 3000 kwa kuwatumia mabalozi mbalimbali.
Amesema BOT imefanya utafiti nini kinachosababisha  kukopa bila kuzingatia mambo muhimu ikiwa ni pamoja na kukopa kwenye taasisi zilizopewa leseni na BOT kwani inakuwa ni rahisi kufuatiliwa pindi inapotoka kwenye mstari  na kuweza kurudishwa.
Amesema pia watanzania watambue wanapotaka mkopo kuzingatia vigezo na masharti  kwa kusoma mikataba ya mkopo husika, kuielewa na kutafakari vizuri na pia kuchukua nakala ya mkataba anaouingia.
Kadhalika amesema ni muhimu wakati wa kukopa kurejesha kwa wakati na wanapokutana na malalamiko yoyote watoe taarifa kwenye dawati la kupokea malalamiko lililoko BOT.
Amesema pia wanapokopa wakope kwa maendeleo kwa ajili ya shughuli za uzalishaji ambazo zitasaidia kufanya marejesho.
“Tumekutana na changamoto ya watanzania kukopa na kupeleka fwdha kwenye sherehe hivyo kupitia kampeni hiyo tunaenda kumzindua mtanzania ili ajue vigezo na masharti lengo likiwa kumlinda mlaji” amesema.
Amesema kwa siku 12 zilizobakia kwa mwezi huu kampeni inaelekea Kinondoni na Ubungo na siku za mbeleni wanaweza kufikiria kuifikisha maeneo mengine.

You Might Also Like

Kamishna TRA Atua Kwa Malasusa Kushirikiana Elimu Kwa Mlipa Kodi

Dkt. Komba: Mfumo wa kidijitali utaleta tija kwa mkulima

China Yaendelea Kunufaisha Afrika, Wakati Marekani Ikikatiza Uwekezaji Katika Bara Hilo

LHRC Kushirikiana  Na JOWUTA Kuwajengea Uwezo Wanahabari Katika Masuala Ya Haki Zao Na Sheria Za Kazi

Trilioni 11.5 Zimetumika Miradi Ya Maendeleo Kigoma

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article WCF Yaleta Utulivu Mahala Pa Kazi – Katambi
Next Article Tanzania Kidedea Tuzo Ya Mashindano Ya Kimataifa  Usalama wa Barabara
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?