MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: China yatoa elimu ya ujenzi kwa wanafunzi Baobab
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > China yatoa elimu ya ujenzi kwa wanafunzi Baobab
Habari

China yatoa elimu ya ujenzi kwa wanafunzi Baobab

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Baobab iliyoko Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wamenufaika na elimu ya vitendo ya ujenzi iliyotolewa na Kampuni ya China Communication Construction (CCCC).
Ofisa Elimu Taaluma kutoka Halmashauri ya Bagamoyo, Juma Yusuph ameeleza hayo baada ya kampuni hiyo kuhamasisha wanafunzi hao kuingia kwenye taaluma ya uhandisi wa ujenzi.
“Kwetu sisi ni faraja. Inaleta chachu kwa wanafunzi hususan wanaosoma masomo ya sayansi kwa kuzingatia maendeleo mengi yanakuja kutokana na ufanisi mkubwa katika sayansi.
“Hii itatusaidia kuhamasisha wanafunzi kuwa chachu ya kuweza kufaya vizuri kwenye sayansi, kujiingiza moja kwa moja katika tasnia ya uhandisi kwenye ujenzi wa barabara na mawasiliano,” amesema.
Amesema dunia sasa ipo katika mfumo wa sayansi na teknolojia unaohitaji wanasayansi wengi waweze kufanikisha maendeleo kwani nchi haiwezi kuendelea bila kuwa na wataalam wa sayansi wanaoweza kufanya miradi mingi itakayoifanya nchi ipige hatua.
Naye Naibu Meneja wa CCCC, Li Yuijang amesema kampuni hiyo imekwenda shuleni hapo kuwafundisha wanafunzi kwa vitendo utaalam wa ujenzi, na mbinu zitakazowasaidia katika maisha yao ya baadaye.
Mwalimu Mkuu katika shule hiyo ya Baobab, Venance Wangoha amesema wameweza kushuhudia kampuni hiyo ikionyesha kazi inazozifanya nchini kuhusiana na uimarishaji wa miundombinu ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wanafunzi kusoma sayansi.
Amesema wahandisi hao kutoka China wameonyesha vifaa wanavyotumia katika kutengeneza miundombinu kwa wanafunzi.
Mwanafunzi Amor Bayumi amekiri kujifunza njia mbalimbali za kutengeneza madaraja ambayo yatapita juu ya bahari ama katika ardhi ambayo imepata dhoruba ya kimazingira ikiwemo mpasuko wa ardhi.
Pia mwanafunzi mwingine wa kidato cha sita shuleni hapo, Amrat Haishaul amesema kupitia mafunzo hayo, yamewahamasisha kuwa hata kama wanasoma kutakuwa na ajira pindi watakapomaliza masomo yao.

You Might Also Like

Mgahawa unaotembea fursa kwa vijana, kutoa huduma ya unywaji wa kahawa

Watafiti Mradi Wa  AGRISPAK kutoka SUA Waanza Uandaaji Wa Vitabu Vidogo

Polisi Yaimarisha Usalama Timu za Simba na Yanga Kesho

Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria

TPHPA ina mchango mkubwa utoshelevu wa chakula – Profesa Ndunguru

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Sera mpya ya viwanda kuzinduliwa
Next Article DIT kudhibiti nzi wa maembe kisasa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mramba Afungua Mafunzo Ya Teknolojia Ya Nishati Jua Kwa Watalaam
Habari August 7, 2025
Mbegu Bora za Miwa Zenye Tija ya Tani 200 kwa Hekta Zaendelea Kuwanufaisha Wakulima
Habari August 7, 2025
Mbegu Bora za Mpunga Zazalishwa TARI Dakawa, Ifakara
Habari August 7, 2025
Mtego wa Inzi Wa Matunda Suluhisho Salama kwa Wakulima
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?