MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari

BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeweka mkakati mahsusi wa ununuzi wa dhahabu tokea Oktoba mwaka jana 2024, ili kuwawezesha wachimbaji wakubwa na wadogo kuuza dhahabu moja kwa moja kwa benki hiyo kwa bei ya ushindani ya kimataifa.
Ofisa kutoka Idara ya Masoko ya Fedha, Rehema Kassim amemweleza hayo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea banda la BoT katika Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mjini Geita,
Habari Picha 9522
Amesema mpango huo ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria ya Madini, kifungu cha 59, kinachowataka wamiliki wa leseni za uchimbaji kuuza angalau asilimia 20 ya dhahabu yao kwa BoT.
“Wachimbaji wana motisha ya kupata punguzo la malipo ya mrabaha kutoka asilimia sita hadi nne, na ada kutoka asilimia moja hadi sifuri,” amesema Kassim.
Habari Picha 9523
Ameongeza kuwa BoT imewawekea wachimbaji urahisi zaidi kwa kuwa sasa wanaweza kuuza hadi asilimia 100 ya dhahabu yao kwa benki hiyo.
Uwasilishaji wa dhahabu BoT unafanyika kupitia kampuni za uchenjuaji ambazo tayari zimesaini mikataba na BoT. Kampuni hizo ni Geita Gold Refinery (GGR) ya Geita, Mwanza Precious Metals Refinery, na Isographica ya Dodoma  uteuzi wa kampuni hutegemea ukaribu wa eneo la uchimbaji.
Kwa mujibu wa sheria, BoT inakusanya dhahabu kwa lengo la kuongeza akiba ya taifa ya fedha za kigeni, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha uchumi wa nchi.
Kupitia maonesho haya, BoT inatoa elimu kwa wananchi kuhusu jukumu lake la msingi katika kuhifadhi akiba ya fedha za kigeni, ambapo dhahabu ni mojawapo ya nyenzo kuu.
Katika hatua nyingine, Meneja wa Idara ya Mawasiliano wa BoT, Vicky Msina, amemkabidhi Waziri Mkuu Majaliwa zawadi ya sarafu ya madini ya fedha  yenye thamani ya Sh. 50,000 kama kumbukumbu.
Aidha, amemwomba Waziri Mkuu kuwa “mwalimu” wa BoT kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utunzaji wa noti na sarafu.

You Might Also Like

VETA Mikumi Yatengeneza Mashine Ya Kuchakata Majani Ya Mifugo

Silaa: Akili Mnemba, Roboti kuongeza ufanisi,ubunifu 

Jaffo Aagiza Kufufuliwa Vilivyokuwa Viwanda Vya Serikali

Rais Samia aipongeza TPHPA, kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi, Watendaji

Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Next Article Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?