MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane
Habari

Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MTEKNOLOJIA wa chakula kutoka Bodi ya Maziwa Tanzania, Rajilan Hillal amesema Bodi hiyo imetumia fursa ya Maonyesho ya Nane Nane Kitaifa kutoa mafunzo kuhusu ubora na usalama wa maziwa kwa wadau mbalimbali wa sekta hiyo.
Maonesho hayo yanaendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Hillal amesema mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha wadau kutambua maziwa salama, yasiyoharibika na yaliyo bora kwa afya ya mlaji, ili waweze kuzalisha na kusindika kitaalamu.
“Tunawafundisha pia namna ya kusindika mazao makubwa mawili yanayotumika zaidi nchini, ambayo ni mtindi wa kawaida na mtindi ulioboreshwa. Lengo letu ni kuhakikisha wananchi wanapata maziwa yaliyo salama na yaliyosindikwa kitaalamu,” amesema.
Amesema changamoto kubwa ni kutowafikia Watanzania wote kutokana na upungufu wa rasilimali, lakini amewashauri wananchi kutumia maziwa yaliyosindikwa yanayopatikana kwenye viwanda vya ndani kwa kuwa ni salama zaidi.
“Tuna jumla ya viwanda 187 vinavyosindika maziwa nchini, vikiwemo vidogo, vya kati na vikubwa. Hivyo ni muhimu wananchi waachane na matumizi ya maziwa yasiyo salama yanayouzwa mitaani, hasa yale yanayohifadhiwa kwenye vyombo visivyo rafiki kama vile machupa ya maji,” amesema.
Hillal amesisitiza kuwa matumizi ya maziwa yasiyo salama yanaweza kuhatarisha afya ya mlaji, na hivyo ni muhimu wananchi kuwa makini katika kuchagua maziwa wanayoyatumia kila siku.

You Might Also Like

JAB Kusimamia  Mfuko wa Mafunzo kwa Waandishi

Tulia Atoa Taarifa Kifo Cha Ndugai

Uongozi CHADEMA Kanda Ya Kati Upo Imara

Kamati YA Siasa Yaendelea Kukagua Miradi Ya Maendeleo Temeke

Wakulima Waomba Watafiti Wa  AGRISPAK, Kuwatafutia Mbinu Kukabili Nzi Weupe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Balozi wa Tanzania Nchini Italy Afurahishwa  Ubunifu wa TPHPA Maonesho ya Nanenane
Next Article Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?