Na Mwandishi Wetu
BOTSWANA: NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko anaiwakilisha Serikali katika sherehe za uapisho wa Rais Mteule wa Botswana Gideon Duma Boko zitakazofanyika Katika Uwanja wa Taifa wa nchi hiyo, leo Novemba nane, 2024.
Akiwasili katika Uwanja wa ndege wa Gaborone, Dkt. Biteko amepokelewa na Katibu Mkuu wa Vijana, Jinsia, Utamaduni na Michezo, Bridget John, Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, James Bwana pamoja na maofisa wengine waandamizi wa Nchi hiyo.

Boko ni Rais wa Sita Botswana kupitia chama cha Umbrella for Democratic Change.
Uchaguzi Mkuu nchini Botswana ulihitimishwa Oktoba 30, 2024 ambapo Rais Mteule Boko aliibuka mshindi katika uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo.