MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Baraza La Wafanyakazi Ni Kama Bunge – Magoiga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Baraza La Wafanyakazi Ni Kama Bunge – Magoiga
Habari

Baraza La Wafanyakazi Ni Kama Bunge – Magoiga

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: “BARAZA la Wafanyakazi ni chombo cha kisheria chenye dhamana ya kutimiza wajibu kama Bunge la Wafanyakazi kwa ngazi ya taasisi, pia kama ilivyo Wabunge kwa ngazi ya Majimbo maana linawakilisha mawazo ya wengi,”.
Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro Stephen Magoiga, amesema  hayo alipokuwa akifungua kikao cha baraza la wafanyakazi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi ( CMA) kilichofanyika Mkoani Morogoro.
Magoiga amesema jukumu la msingi la Baraza la wafanyakazi ni kushauri menejimenti katika maeneo mbalimbali ya utekelezaji wa majukumu ambayo taasisi ina wajibika kwa umma na kujadili bajeti ya taasisi na utekelezaji wake kwa kila mwaka wa fedha.
Ameliagiza baraza hilo kufanya wajibu wake  kwa ujasiri na umakini ili kulinda haki na wajibu wa wale waliowachagua kwa maslahi mapana ya Taifa.
Vile vile amewataka wajumbe wote kusoma kwa makini mkataba wa baraza hasa sehemu ya wajibu ili mara zote wanapokutana wajue wanayopaswa kuyafanya.
“Sisi kama watumishi wa Umma tunawahakikishia watanzania usalama kazini na wawekezaji watapata uhakika wa mazingira rafiki ya uwekezaji nchini,” amesema.
Pia amesema mahakama itaendelea kutoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuhakikisha tume inatekeleza wajibu wake katika kutoa haki kwa jamii ya wafanyakazi na waajiri.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa CMA, Usekelege Mpulla, amemshukuru Jaji Stephen Magoiga na kumhakikishia kuendelea kutimiza wajibu kwa kufuata taratibu na sheria.

You Might Also Like

Bodi ya Bima ya Amana Yatoa  Bil 9.07 , Fidia Kwa Wateja Wa Benki Saba   Zilizofilisika

VETA Mtwara Yawafundisha Wanafunzi Uongezaji Thamani Kwenye Korosho, Mwani

Nchimbi Agongelea Nyundo Kwa Wagombea Watoa Rushwa

Tanzania, Ufini Kushirikiana Teknolojia Za Kisasa Sekta ya Misitu

SOKO LA MADINI LA 43 LA ZINDULIWA TUNDURU RUVUMA.

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article WCF Yatakiwa Kuongeza Nguvu Kusajili Waajiri
Next Article TUCTA Yaanza Maandalizi Ya Mei Mosi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?