MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee
Habari

Aloe Dorotheae, Mmea Unaopatikana Tanzania Pekee

Author
By Author
Share
3 Min Read

Hutibu Magonjwa Mbalimbali, TPHPA Wafunguka

Na Lucy Ngowi

MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA), imesema mmea wa Aloe dorotheae unaopatikana nchini Tanzania pekee hutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu na mifugo.

Meneja wa Idara ya Utambuzi wa Mimea kutoka TPHPA, Dkt. Neduvoto Mollel amesema hayo alipozungumza na Mfanyakazi Tanzania kuhusu jukumu la Kitaifa la kuhifadhi sampuli na taarifa zote za bioanuwai ya mimea ya Tanzania kupitia Kitengo cha Taifa cha Kuhifadhi ya sampuli za Mimea.

Amesema mmea huo pia kwa kizigua hujulikana kwa jina la Kikori, ambao hutumika kama kiungo muhimu kwenye pombe ya kienyeji kutokana na ladha yake chungu.

“Kutokana na manufaa ya mmea huu kwa matibabu ya binadamu, hitaji lake huongezeka siku hadi siku.  Wananchi wa Kang’ata huvuna kulingana na mahitaji yao na bila kufikiria kuwa unaweza ukaisha,” amesema.

Amesema walitoa elimu kwa jamii ya eneo hilo kuhusu mmea huo kuwa ni wa kipekee katika eneo lao, hivyo wautunze.

“Tuliwapa ushauri kuacha  uvunaji usio endelevu kwa kuwa utasababisha mmea huu kupotea kwenye eneo lake la asili,” amesema.

Akiuelezea mmea huo amesema unapatikana nchini Tanzania pekee.

“Haupatikani katika nchi nyingine yeyote duniani ukiwa katika maeneo ya asili. Kama upo ni kwa kupelekwa kuoteshwa kama mapambo bustanini au kwa ajili ya matumizi ya dawa majumbani.

“Aloe dorotheae ni ukoo mmoja (Aloaceae) na Aloe vera.  Asili ya Aloe vera ni Rasi ya Arabia Peninsula ya kusini-mashariki ya Arabia katika Milima ya Hajar ingawaje sasa unalimwa sehemu nyingi  dunia kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Asili ya Aloe dorotheae ni Tanzania,” amesema.

 Amesema nchini Tanzania Aloe dorotheae hupatikana Mkoa wa Tanga, wilaya ya Handeni katika Kata ya Kang’ata na sio penginepo.

Hukua kwenye miamba yenye udongo mdogo tu unaotokana na majani yanayooza juu ya miamba.

Amesema hadi sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na aina takribani 14,000, kati ya hizo takriban 1500 ni aina ambazo hazipatikani popote duniani isipokuwa Tanzania.

Amesema TPHPA ina jukumu kubwa la Kitaifa la kuhifadhi sampuli na taarifa zote za bioanuwai ya mimea ya Tanzania kupitia Kitengo chake cha Taifa cha Kuhifadhi ya sampuli za Mimea.

“Inahifadhi sampuli za mimea yote ya Tanzania na Taarifa muhimu zinazoambatana na sampuli hizo.

“Zaidi ya kuhifadhi sampuli kavu, TPHPA imeanzisha bustani ya kuhifadhi mimea hadimu na yenye matumizi makubwa kwa tiba ya binadamu kwa ajili ya muendelezo wa kizazi cha mimea hiyo na kwa ajili ya matumizi endelevu ya vizazi vya sasa na vya baadae ya Watanzania,” amesema.

You Might Also Like

VETA Mikumi Yatengeneza Mashine Ya Kuchakata Majani Ya Mifugo

Theluthi mbili ya nguvu kazi ya taifa ipo kwenye kilimo

Kassim Majaliwa Mgeni Rasmi Miaka 30 VETA

Trilioni 1.2 Kumaliza Tatizo la Maji Dar

Majaliwa Asisitiza Serikali Itaendelea Kuboresha Mazingira Ya Uwekezaji

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TPHPA Kuipokea Ndege Yake
Next Article Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Hali Ya Ulinzi Na Usalama Wa Mipaka Ni Salama
Habari May 22, 2025
Ulega Ataka Ushirikiano Miradi Ya Kimkakati Ikamilike Kwa Wakati
Habari May 22, 2025
TPHPA Kuipokea Ndege Yake
Habari May 22, 2025
Wanaosimamia Mitandao Ya Serikali Wadhibiti Usalama Wake
Habari May 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?