MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Uongozi OUT Waahidi Kuboresha Mazingira ya Kazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Uongozi OUT Waahidi Kuboresha Mazingira ya Kazi
Habari

Uongozi OUT Waahidi Kuboresha Mazingira ya Kazi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Vincent Mpepo (OUT)
DAR ES SALAAM. Uongozi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) umeahidi kuendelea kuboresha mazingira ya kazi kadiri ya uwezo wa kifedha wa chuo, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza ufanisi wa kazi na mapato ya taasisi.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa gari jipya la ofisi yake jijini Dar es Salaam, Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Alex Makulilo, amesema chuo kinatambua changamoto zilizopo kwenye mazingira ya kazi, na kitaendelea kuzitatua hatua kwa hatua kwa kutumia rasilimali za ndani.
Habari Picha 9977
Profesa Makulilo amebainisha kuwa ununuzi wa gari hilo umefadhiliwa kwa mapato ya ndani ya chuo, na aliipongeza timu yote iliyosimamia mchakato huo kwa kufuata taratibu na kuhakikisha thamani ya fedha inazingatiwa.
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Huduma za Mikoa na Teknolojia za Kujifunzia, Profesa Leonard Fweja, amesema gari hilo litarahisisha majukumu rasmi ya Makamu Mkuu wa Chuo, hasa katika kusimamia vituo vya OUT vilivyopo nchi nzima.
Kwa upande wake, Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu, Dkt. Dunlop Ochieng, ametaja upatikanaji wa gari hilo kuwa ni matokeo ya mshikamano na kujituma kwa wafanyakazi wa chuo.
Benjamin Bussu, Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo, amesema mchakato wa manunuzi ulianza Februari 2025 na ulifuata taratibu zote, ikiwemo kupata kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi.
Gari lililonunuliwa ni aina ya Toyota Land Cruiser yenye thamani ya Sh. milioni 386, na linatarajiwa kuimarisha shughuli za kiutendaji za viongozi wa chuo.
Bussu amesisitiza umuhimu wa kulitunza gari hilo na kulitumia kwa uangalifu kwa maslahi ya taasisi na usalama wa viongozi wake.

You Might Also Like

Dkt. William Ruto Aipongeza NSSF Tanzania Kwa Uwekezaji wa Dola zaidi ya Milioni 51 Nairobi

Samia Mgeni Rasmi Siku Ya Mashujaa

Washauri Serikali Kutumia Fedha Za Miradi

BoT: Tumia Taasisi za Fedha Halali kwa Usalama wa Kifedha

Watumishi wa Umma Watakiwa Kuwa na Nidhamu, Ubunifu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Elimu ya Ufundi Yachangia Maendeleo ya Taifa – VETA
Next Article Waziri Mkuu Ashiriki Kumuombea Baba Wa Taifa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ziwa Ngozi Lavuta Mamia Sabasaba, Wageni Washangazwa Na Ramani Ya Afrika Juu Ya Mlima
Habari July 9, 2026
Shirika La Uzalishaji Mali La Polisi Kujenga Vituo Vya Ukaguzi Wa Vyombo Vya Moto
Habari July 9, 2026
Watumishi 7881 Watakaostaafu 2026/27 Watambuliwa Kupitia Kampeni Ya Tunalipa Jana-PSSF
Uncategorized July 8, 2026
Katambi Apongeza Zimamoto Kwa Uwekezaji Wa Vifaa Vya Kisasa
Uncategorized July 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?