MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, amelipongeza Jeshi la Magereza kwa hatua kubwa ya kurasimisha ujuzi wanaoupata wafungwa kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), hali inayowawezesha kupata ajira au kuanzisha shughuli za kujitegemea baada ya kumaliza vifungo vyao.
Ametoa pongezi hizo wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 64 ya kuanzishwa kwa Jeshi la Magereza, yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania kilichopo Ukonga, jijini Dar es Salaam.
Habari Picha 9171
“Ninatoa pongezi za dhati kwa Jeshi la Magereza kwa mafanikio haya. Huu ni mpango kazi wenu na tumeona faida zake. Vijana waliokuwa hapa wametoa ushuhuda namna walivyonufaika na mafunzo haya ya stadi za kazi.” amesema.
Ameeleza kuwa kupitia mitaala mipya ya mafunzo ya amali na stadi za kazi, Jeshi hilo limefanikiwa kuwafikia na kunufaisha zaidi ya wafungwa 5,000, ambapo baadhi yao tayari wamepata ajira au wameanzisha biashara binafsi baada ya kutoka gerezani.
Habari Picha 9172
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Jumanne Sagini amelipongeza Jeshi hilo kwa umahiri wake wa kutafsiri na kutekeleza maelekezo ya Serikali pamoja na viongozi mbalimbali, hata mara nyingine bila kuwezeshwa kifedha moja kwa moja kutoka serikalini.
Sagini amesema Jeshi la Magereza limeendelea kufanyia kazi mapendekezo ya Tume ya Rais ya Maboresho ya Vyombo vya Haki Jinai, ikiwa ni pamoja na kuboresha programu za urekebishaji wa wafungwa.
“Ujuzi wanaoupata wafungwa kupitia mafunzo haya ni wa muhimu sana katika kuwawezesha kufanya shughuli halali za kujikimu mara baada ya kurudi kwenye jamii, na hivyo kusaidia kupunguza uwezekano wa kurejea katika makosa.” amesema.
Habari Picha 9173
Awali Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Jeremiah Katungu, ameeleza kuwa Jeshi hilo limefanikiwa kuandaa mitaala mipya 10 kwa ajili ya kuboresha utoaji wa mafunzo stahiki kwa watumishi wake na kwa wafungwa.
Mitaala hiyo imeandaliwa kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali zikiwemo Chuo cha Ustawi wa Jamii, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), pamoja na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW).
“Tumeandaa pia Mwongozo wa Programu za Urekebishaji kwa Wafungwa. Mwongozo huu umeweka misingi thabiti na utaratibu wa mapokezi, tathmini, urekebishaji, pamoja na kuwaandaa wafungwa kurejea kwenye jamii wakiwa raia wema,” amesema.

You Might Also Like

Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato

Jisajilini mapema mpate mbolea ya ruzuku

Polisi Kufuatilia Wanaochuja Mafuta Na Mifuko Kwenye Malori

Tanzania Na Italy Wasaini Makubaliano Kuongeza Ubora Mafunzo Ya Ukarimu

Utiaji Saini Mkataba Wa Ujenzi Jengo La TUGHE Wafanyika

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
Bodi Ya  Bima Ya Amana Yapata Mkurugenzi  Mkuu
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?