MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kutoka 1975 hadi 2025: TUCTA Yatimiza Ndoto Ujenzi Jengo La Biashara Arusha
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kutoka 1975 hadi 2025: TUCTA Yatimiza Ndoto Ujenzi Jengo La Biashara Arusha
Habari

Kutoka 1975 hadi 2025: TUCTA Yatimiza Ndoto Ujenzi Jengo La Biashara Arusha

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
ARUSHA: RAIS wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhokya, amesema ni nadra kukuta vyama vya wafanyakazi vikimiliki mali yenye thamani kama wanayomiliki sasa.
Habari Picha 8928
Nyamhokya amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la biashara jijini Arusha, lililozinduliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu),
“Miaka ya nyuma, mwajiri akisikia viongozi wa vyama wanakuja, aliona kama ni vita. Lakini viongozi tuliopo sasa, tangu 2017, tulikubali kubadilika tumeamua kutumia njia ya majadiliano na serikali.” amesema Nyamhokya.
Habari Picha 8943
Amesema kupitia usimamizi wa kisasa na ushirikiano na taasisi za serikali, TUCTA imeweza kukarabati mali nyingi zilizokuwa zimechakaa, ikiwa ni pamoja na chuo chao kilichoko Mbeya, nyumba kubwa jijini Dodoma, na sasa jengo hilo la biashara jijini Arusha.
“Katika jengo hilo la biashara kuna huduma mbalimbali ikiwemo hoteli, maduka ya vifaa vya magari, vitabu, nguo za wanawake, wanaume na watoto, pamoja na bidhaa mchanganyiko hatua iliyolenga kuinua mapato ya shirikisho na kutoa ajira,” amesema.
Habari Picha 8933
Akielezea historia ya jengo hilo amesema, “Jengo hili la biashara ni la aina yake kwa Arusha. Tulianza ujenzi wake mwaka 1975 lakini kwa muda mrefu ulisimama. Tulipofika 2017, tukaamua kwa pamoja kulifufua. 2022 tukapata mkandarasi mpya. Sasa limekamilika kwa asilimia kubwa, lifti pekee ndio bado,” amesema.
Kwa upande mwingine amesema, Kwa sasa, shirikisho hilo lina vyama 16, kutoka vyama 13 vya awali.
Amevitaja vyama vipya vilivyopokelewa ni pamoja na Chama cha Wafanyakazi wa Vyombo vya Habari (JOWUTA), Chama cha Wafanyakazi wa Sekta ya Ulinzi Binafsi (TUPSE) na Chama cha Wafanyakazi wa Huduma za Viwandani Tanzania (TASIWU).
Habari Picha 8936
Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa umma iliyotolewa Julai mwaka huu, kama alivyoahidi katika sikukuu ya Wafanyakazi ijulikanayo kama Mei Mosi mwaka huu 2025.
“Mama ameonyesha upendo kwa wafanyakazi. Aliahidi, ametekeleza. Sasa tunajisikia salama. Ni nafuu kuwa na kiongozi anayesikiliza unagonga mlango, anafungua,” amesema.
Habari Picha 8937
Pia amemshukuru Waziri Ridhiwani kwa kuendelea kushirikiana nao kwa karibu. “Tunakuombea uchaguzi uende salama na Rais Samia akupange katika wizara hii hii. Umeonesha dhamira ya kweli kwa wafanyakazi,”.
Katika kudumisha mshikamano, TUCTA imeandaa vyeti maalum kwa ajili ya vyama vyote vya wafanyakazi, ikiwa ni njia ya kutambua mchango wao katika maendeleo ya shirikisho hilo.

You Might Also Like

TARI Yawafikia Wakulima Kilosa, Kilimo Shadidi Cha Mpunga

Si ruhusa kufuga, kuchunga, kuvua maeneo ya umwagiliaji

Profesa Mkenda Aitaka TAEC Kusomesha Watumishi

Ndunguru: Mabadiliko Ya Tabianchi Yanachangia Kuwepo Kwa Magonjwa, Wadudu Kwenye Mazao

Sera mpya ya viwanda kuzinduliwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Nchi Za SADC Zahimizwa Kutunza, Kulinda Amani
Next Article Ridhiwan Azindua Jengo La Biashara La TUCTA-Arusha
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?