MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Dodoma Yang’ara Katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Dodoma Yang’ara Katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani
Habari

Dodoma Yang’ara Katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani

Author
By Author
Share
3 Min Read
Wakulima Wafaidika na Mapato Yaongezeka
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MKOA wa Dodoma umeendelea kung’ara katika utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani, ambapo zaidi ya tani 1,000 za mazao ziliuzwa kupitia mfumo huo.
Mrajis wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Dodoma, Joseph Chitinka amesema leo katika viwanja vya maonesho vya Nanenane Nzuguni Dodoma.
Amesema mafanikio hayo yamewanufaisha wakulima kwa kuongeza kipato chao, huku serikali ikipata mapato ya kutosha kutokana na shughuli hizo.
Amesema mfumo huu umeleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa wakulima wadogo ambao sasa wanaweza kuuza mazao yao kwa bei nzuri na kwa uhakika.
“Tumeweza kufanya transformation ya maisha hasa ya wakulima wadogo kutoka hatua moja kwenda nyingine,” amesema.
Amesema Mkoa wa Dodoma una jumla ya vyama 126 vya ushirika, ambapo kati ya hivyo, 27 vinajihusisha moja kwa moja na kilimo. Pia, kuna zaidi ya SACCOs 70 zinazojumuisha zile za mahala pa kazi pamoja na za kijamii zinazowahudumia wananchi wa kawaida, wajasiriamali, na wafanyabiashara.
“Mkoa huu umeendelea kuimarika katika uzalishaji wa mazao matano makuu ambayo ni ufuta, choroko, mbaazi, dengu na zabibu.
“Zabibu inatajwa kuwa ni zao la kipekee na fahari ya mkoa huo. Wadau wa zao hilo wamefanikiwa kuongeza thamani kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali kama mchuzi wa zabibu kwa ajili ya kutengeneza wine,” amesema..
Amesema hadi sasa, kuna viwanda viwili vinavyoongeza thamani ya zabibu mkoani Dodoma.
Amesema mchuzi wa zabibu umevutia soko kubwa, ikiwemo kwa wafanyabiashara wakubwa wanaousafirisha hadi nje ya nchi kwa ajili ya kutengeneza wine.
Katika maonyesho ya mwaka huu, vyama vya ushirika vya zabibu vimeshiriki kikamilifu na kuuza bidhaa zao kwa wingi, jambo lililowawezesha kupata kipato na kuimarika kiuchumi.
Aidha, mkoa wa Dodoma umeanza maandalizi ya ukusanyaji wa mazao ya mbaazi, choroko na dengu kwenye maghala mbalimbali, na minada inatarajiwa kuanza katikati ya mwezi huu.
Chitinka amesema ushirika wa kuweka na kukopa umekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya kiuchumi ya wakazi wa Dodoma, ambapo SACCOs mbalimbali zimeweza kutoa mikopo kwa wanachama, kuwainua wajasiriamali na wafanyabiashara, na kuhamasisha watu zaidi kujiunga na vyama vya ushirika.

You Might Also Like

Masauni Akabidhi Polisi Magari 77

TARI Yaja Na Jawabu 88 Juu Ya Tindikali, Chumvi Kwenye Udongo

Rais Samia na maadhimisho ya miaka 60 ya JWTZ

Serikali Kuendelea Kuboresha Sheria za Ulinzi wa Watoto

SADC Yatathmini Maendeleo ya Mpango wa RISDP Katika Mkutano wa 45 Madagascar

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Samia, Nchimbi Kuchukua Fomu Ya Urais Kesho
Next Article Sheikh wa Mkoa, ‘Wanaotoa Rushwa Msiwachague’
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Fema Mining & Drilling Mfano wa Kuigwa – Musukuma
Habari September 23, 2025
Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa
Habari September 23, 2025
Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa
Habari September 23, 2025
Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?