MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Habari

Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MKURUGENZI Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Hassan Saidy amesema kufikia mwaka 2034, zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanaweza kuwa wanatumia nishati safi ya kupikia, kutokana na mipango madhubuti ya Serikali na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanyika.
Akizungumza katika maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane 2025 yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni, Jijini Dodoma, Saidy amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imeanza kutekeleza kwa vitendo Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne sasa.
Amesena juhudi hizo zimehusisha uwekezaji mkubwa wa rasilimali fedha, muda na teknolojia, hatua ambayo imeongeza mwamko wa wananchi kutumia teknolojia za kisasa za nishati safi.
Amewashauri Watanzania kuchagua aina ya nishati safi inayolingana na uwezo wao wa kifedha, kwani fursa za kuchagua zipo.
“Nishati safi ni pamoja na umeme, gesi ya majumbani, gesi asilia, mkaa mbadala, kuni mbadala na gesi vunde. Aina hizi zinapatikana lakini matumizi yake yanategemea hali ya uchumi wa mtu binafsi. Ndiyo maana tunasisitiza watu kuchagua kwa uangalifu kulingana na uwezo wao,” amesema.
Ametaja baadhi ya miradi mikubwa iliyotekelezwa na Wakala huo ikiwemo, Kuwezesha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kutumia nishati safi ya kupikia katika kambi 22 nchini, kwa gharama ya Sh. Bilioni tano.
Uwezeshaji wa maeneo 211 ya Jeshi la Magereza kutumia nishati safi, kwa gharama ya Sh. Bilioni 35.2.
Kusaini mkataba na Kampuni ya Taifa ya Madini (STAMICO) kwa ajili ya uzalishaji wa mkaa mbadala.
“Hii inaonesha dhamira ya Serikali kuhakikisha taasisi zake nazo zinakuwa mfano katika matumizi ya nishati safi,” amesema.
Amehamasisha wananchi kutembelea banda la REA lililopo katika eneo la Wizara ya Nishati, Hema Na. 2 (Government Pavilion No. 2), upande wa Kusini Mashariki wa viwanja vya maonesho ya Nzuguni, ili kupata elimu kuhusu nishati safi na teknolojia zake.
Ameeleza pia kuhusu fursa zinazotolewa na Serikali kupitia REA, ikiwa ni pamoja na utoaji wa mikopo nafuu kwa ajili ya ujenzi na uendelezaji wa vituo vidogo vya bidhaa za mafuta (Petroli na Dizeli) vijijini, pamoja na maendeleo makubwa ya usambazaji umeme katika vijiji na vitongoji nchini kote.

You Might Also Like

Tunatatua Malalamiko Ya Wateja – Kaguo

TARI Yawafikia Wakulima Kilosa, Kilimo Shadidi Cha Mpunga

Walimu Wanaofundisha Lugha Ya Kichina Tanzania Wakutana

FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara

Katambi aitaka BRELA kuharakisha urasimishaji wa biashara

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane
Next Article TAMWA Yawawezesha Wanawake Kupitia Mradi wa Nyuki
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?