MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: CCM Yasitisha Ratiba ya Uchaguzi wa Maoni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > CCM Yasitisha Ratiba ya Uchaguzi wa Maoni
Habari

CCM Yasitisha Ratiba ya Uchaguzi wa Maoni

Author
By Author
Share
2 Min Read
  • Wagombea Watakiwa Kuvuta Subira
Na Danson Kaijage
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimeahirisha rasmi mchakato wa kuwateua wagombea wa nafasi za ubunge na udiwani, mchakato uliokuwa umepangwa kufanyika leo Julai 19, sasa ukisogezwa mbele hadi Jylai 28, mwaka huu 2025.
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi,  Amos Makala alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo.
Ameeleza kuwa hatua hiyo imechukuliwa ili kutoa muda wa kutosha kwa chama kufanya uchambuzi wa kina kwa kila mgombea kutokana na idadi kubwa ya waliotangaza nia ya kugombea nafasi hizo.
“Tumelazimika kusogeza mbele ratiba hii kwa sababu ya wingi wa waombaji. Tunataka tuhakikishe tunafanya kazi ya uchambuzi kwa makini, kwa haki na kwa kuzingatia sifa stahiki za wagombea wote,” amesema.
Kwa mujibu wa Katibu huyo, kabla ya kufanyika kwa kura za maoni mnamo Julai 28,, kutatanguliwa na vikao muhimu vya uongozi wa juu wa chama.
Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kinatarajiwa kufanyika Julai 26 , na siku hiyo hiyo kufuatiwa na kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.
Aidha, Makala amewataka wagombea wote waliokwisha tangaza nia kuwa watulivu na kuendelea kufuata taratibu za chama huku wakijiepusha na kampeni za mapema au vitendo vya uchochezi vinavyoweza kuvuruga utaratibu wa chama.
“Ni vyema wagombea wakaonesha uvumilivu na nidhamu ya hali ya juu. CCM ni chama kinachoongozwa na misingi ya haki, hivyo kila mtu atapata nafasi yake ya kusikilizwa kwa mujibu wa kanuni,” amesema.
Kwa sasa, chama hicho kinasisitiza kuwa kinaendelea na kazi ya kuhakiki majina ya waombaji wote katika ngazi mbalimbali, kuhakikisha wagombea watakaopitishwa ni wale wenye uwezo, uadilifu na wanaokubalika kwa wananchi.

You Might Also Like

Mume na Mke Wafariki Kwa Wivu Wa Kimapenzi

NHIF: Ruksa wanachama kutumia NIDA

Kafulila: Deni La Taifa Ni Himilivu

Kumekucha Uzinduzi wa Washirika wa Tamasha, Tuzo Za Filamu Tanzania 2025

Senene Waongezewa Thamani UDSM

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Uvuvi Wa Kisasa Wainua Mwanza Kiuchumi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Uvuvi Wa Kisasa Wainua Mwanza Kiuchumi
Habari July 19, 2025
Tanzania Yaingia Saba Bora Duniani  Kwa Uzalishaji Wa Pamba Hai
Habari July 19, 2025
Mara Yapaa: Miaka Minne Ya Mafanikio Chini Ya Rais Samia
Habari July 18, 2025
Serikali Yazindua Mafunzo Ya Mtandao Ya Afya Moja
Habari July 16, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?