MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria
Habari

Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: KAMISHNA wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Nyanda Shuli amepongeza Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) kwa kutekeleza kwa vitendo mapendekezo ya mabadiliko ya sheria mbalimbali yanayopendekezwa na wananchi kupitia taasisi na wadau wa haki nchini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam alipotembelea banda la OCPD katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yajulikanayo kama Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam, Kamishna Shuli amesema kazi inayofanywa na ofisi hiyo ni msingi muhimu wa kuhakikisha sheria zinakidhi mazingira halisi ya sasa.
“Ofisi hii inatoa huduma zinazoshabihiana na zetu. Tunapokea maoni ya wananchi kuhusu sheria mbalimbali ambazo zimepitwa na wakati au hazizingatii hali halisi.
“Kwa kawaida, mapendekezo hayo hupitia mchakato mrefu lakini mwisho wa safari huletwa kwenu kwa ajili ya kuandikwa upya au kurekebishwa kabla ya kuwasilishwa bungeni.
“Hii ni hatua muhimu ya kuhakikisha haki na sheria zinakwenda na wakati,” amesema.
Akitolea mfano, Kamishna ameeleza changamoto iliyobainishwa na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Kusini wakati wa uchunguzi uliofanywa mikoani, ambapo sheria ya Uhujumu Uchumi ilionekana kutoendana na mazingira halisi ya maeneo hayo.
Sheria hiyo iliwahusisha wanyama kama swala na digidigi katika makosa ya uhujumu uchumi, hali iliyowafanya wananchi wengi kufungwa bila dhamana kwa makosa yasiyostahili adhabu kali kiasi hicho.
“Ni jambo la faraja kwamba baada ya mchakato mrefu wa ukusanyaji maoni, sheria hiyo sasa imefanyiwa marekebisho kwa kuzingatia uhalisia na malengo halisi ya kulinda wanyama waliolengwa awali, yaani ‘Big Five’. Hili ni zao la kazi kubwa inayofanywa na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria,” amesena.
Kwa upande wake, Mwandishi wa Sheria kutoka OCPD, Happyphania Luena, ametoa shukrani kwa Kamishna Shuli kwa kutembelea banda hilo na kutambua kazi ya ofisi hiyo, akisema kuwa ushirikiano kati ya OCPD na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ni wa mfano na wenye tija kubwa katika kulinda haki na usawa wa kijamii.
“Mbele yako ni Juzuu za Sheria zilizofanyiwa Urekebu toleo la mwaka 2023. Tumezileta hapa kuwaonesha wananchi kazi hii muhimu ya kuhuisha sheria.
“Toleo la mwaka 2002 lilifutwa rasmi baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuzindua rasmi toleo hili jipya. Wananchi wanapaswa kuelewa kuwa sheria ni nyenzo ya maendeleo na si kikwazo,” amesema.
Mchakato wa urekebishaji wa sheria unatajwa kuwa chachu ya uboreshaji wa mifumo ya kisheria nchini, na unaonesha kwa vitendo dhamira ya Serikali kuhakikisha haki, uwajibikaji, na utawala bora vinazingatiwa katika kila hatua ya maisha ya wananchi.

You Might Also Like

Asilimia 22 Ya Vijana Wanakumbwa Magonjwa Yasiyo Ya Kuambukizwa

UTT AMIS Yazindua kampeni ya ‘Kijiwe Mchongo

Magonjwa ya misuli yaongezeka mahala pa kazi-OSHA

Mkandarasi wa mradi wa REGROW, Kilolo  atakiwa kuongeza Kasi.

TPHPA Kuipokea Ndege Yake

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Johari Ataka Ufasili wa Sheria za Uchaguzi Ukamilike
Next Article Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Habari July 12, 2025
Johari Ataka Ufasili wa Sheria za Uchaguzi Ukamilike
Habari July 12, 2025
OCPD Nguzo Kuu ya Utungaji Sheria – Dkt. Ndumbaro
Habari July 12, 2025
Pato la Mwananchi Lapanda Tabora
Habari July 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?