MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA Kihonda Waja Na Mashine Ya Kusaga Chumvi Sabasaba
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA Kihonda Waja Na Mashine Ya Kusaga Chumvi Sabasaba
Habari

VETA Kihonda Waja Na Mashine Ya Kusaga Chumvi Sabasaba

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: CHUO cha Ufundi Stadi (VETA), Kihonda mkoani Morogoro kimetengeneza mashine ya kusaga chumvi, kutoka kwenye mfumo wa mawe iwe kwenye chenga chenga ndogo ndogo.

Mkufunzi Mwandamizi wa Chuo hicho, Fredrick Uliki amesema hayo alipozungumza na Mfanyakazi Tanzania kuhusu changamoto inayowakabili wakulima wa chumvi, katika maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Urick amesema chuo hicho kimetengeneza mashine hiyo baada ya kubaini changamoto iliyokuwa ikiwakabili walimaji wa chumvi katika eneo la Bagamoyo Pwani na Lindi.

“Wanafunzi wetu walifika maeneo hayo wakakuta wakulima wengi wa chumvi hawana kifaa cha kuwarahisishia kusaga chumvi kutoka kwenye mfumo wa mawe iwe kwenye mfumo wa chenga ndogo ndogo ambazo tayari kwa ajili ya matumizi baada ya kuweka dawa ile ya madini joto.

“Kwa hiyo wanafunzi walivyofanya tafiti zao wakaja na mashine hii, na mashine hii sasa baada ya kuona kuna fursa sasa ya kibiashara ya kimataifa hapa tutapata watu wengi watakaohitaji huduma yetu,” amesema.

Amesema inawezekana maeneo mengine pia wana shida ya kusaga chumvi kama ilivyo hayo maeneo mawili, wakaweza kupanua wigo wa huo ubunifu na kuingiza kwenye biashara ili chuo kipate mapato ya kurejesha malighafi ambazo zimetengenezea mashine hiyo.

“Wajasiriamali wa chumvi wakisaga chumvi yao kwa kutumia mashine hii itawaongezea thamani, wataweza kufungasha katika ukubwa wowote na kuuza kwa bei ya juu zaidi, na ikakaa kwa namna ya usafi.

“Tunawakaribisha wajasiriamali hao wafike kwenye banda la VETA, wajionee walete familia zao waweze kusoma VETA,” amesema.

You Might Also Like

Waziri Mkuu Majaliwa Akoshwa Na Tafiti Ya Mhitimu OUT

Chuo Cha Ustawi  Wa Jamii Chawataka Wazazi Kujitokeza Kufundishwa Kuhusu Malezi

TARI Yawaalika Wakulima Kujifunza Teknolojia Bora 88 Mkoani Morogoro

TRAWU Yapigania Wafanyakazi TAZARA Nyongeza Ya Mshahara

Mafunzo ya Ufundi Sasa Kupatikana Popote Kupitia Programu ya VSOMO”

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi
Next Article TAWA Ni Mahali Sahihi Pa Uwekezaji  – Maganja
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mradi Wa Umeme Mpomvu-GGM Kuimarisha Upatikanaji Wa Umeme Na Kuchochea Shughuli Za Kiuchumi Geita- Salome
Habari September 4, 2026
Wahitimu 794 Wa Vyuo Vya Elimu Ya Juu Waomba Kujiunga VETA
Habari September 4, 2026
Taka za saluni zageuka dhahabu ya kijani: COSTECH yamulika safari ya David kutoka wazo hadi hataza
Makala September 4, 2026
Umeme Kubadilisha Maisha Ya Wakazi Wa Kisiwa Cha Jibondo Mafia
Habari September 3, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?