MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina
Habari

Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM:MASHINDANO ya Lugha na Tamaduni za Kichina kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi yanapima kiwango chao cha uelewa ili wapangwe kwa kuzingatia ufaulu wao kuanzia mtu wa kwanza hadi wa nne.

Mwakilishi wa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Flora Magige amesema hayo wakati akifungua mashindano hayo yaliyofanyika chuoni hapo ambayo yamewashirikisha wanafunzi 15 wa Shule za Msingi.

Profesa Magige amesema Mashindano hayo ni kipimo kizuri kwa mwalimu kujua uwezo wa mwanafunzi na kuona ni wapi aweke mkazo zaidi.

Pia amesema suala la ushiriki wa wanafunzi hao ni hatua  muhimu kwa kuwa kila mmoja amejiamini na kushiriki mashindano hayo.

“Ninamtia moyo kila mmoja wenu hata Yule atakayeshika nafasi ya 15, kuna usemi unasema asiyekubali kushindwa sio mshindani, kwangu mimi wote ni washindi endeleeni kupambana bila kukata tama,” amesema.

Amesema amefurahi kusikia mashindano hayo ni watoto wa shule za msingi kwa kuwa inapendeza kuwaona wakishiriki kwa lengo la kujua lugha na tamaduni za kigeni ikiwa ni pamoja na kichina.

Naye Mkurugenzi Mtanzania wa Taasisi ya Kujifunza lugha ya Kichina ya Confucius, Dkt. Mussa Hans amesema katika mashindano hayo wanafunzi wameonyesha vipaji vyao vya kusimulia hadithi, kutoa hotuba, kughani mashairi ya kale na kuimba nyimbo mbalimbali wakitumia ishara mbalimbali na kuonesha hisia zao kuhusu kile wanachokiwasilisha.

“Kutokana na kuimarika kwa uhusiano wa kirafiki kati ya China na Tanzania, wadau wengi wamekuwa wakivutiwa kujifunza lugha na utamaduni wa kichina.

“Tunafurahi sana kuona kwamba wanafunzi wengi zaidi wa shule za msingi wanajifunza kichina katika umri mdogo.

“Tunaamini mbegu hizi zinazopandwa kwa wanafunzi hawa zitachanua na kuzaa matunda bora katika kujenga daraja la kuendelea kuimarisha urafiki kati ya China na Tanzania kwa sasa na baadaye,” amesema.

Amewaambia wanafunzi hao kuwa mashindano hayo yatakuwa ni kichocheo katika kuendelea kujifunza lugha na utamaduni wa kichina.

“Tunaamini kuwa katika kujifunza huku tutaendelea pia kujiimarisha katika kufanya kazi kwa bidii kuanzia katika umri wa utoto kwani hiyo pia ni sehemu ya utamaduni wa wachina,” amesema.

Naye Atka Said mwanafunzi wa darasa la nne katika Shule ya Nira Zanzibar amesema ameshiriki mashindano hayo kwa kuwa anapenda lugha hiyo.

Pia mwanafunzi Baraka Ramadhan wa Shule ya Msingi St. Mathew amesema ameshindana mashindano hayo kwa kuwa lugha hiyo ina utamaduni mzuri ikiwemo kuimba na kucheza.

You Might Also Like

Erio atoa elimu ya bidhaa bandia kwenye mabanda nanenane

Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe

Watafiti, Wabunifu Waendelezwe Wasivunjwe Moyo- Biteko

Rais Samia atoa zaidi ya bil. 2.1 usimikaji wa mifumo, uendeshaji mashauri ya wafanyakazi

Miradi Dodoma Yamkuna Rais Samia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Uchaguzi Mkuu 2025: Majimbo Mapya Nane Yaanzishwa, 12 Yabadilishwa Majina
Next Article SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

FCC Yatoa Elimu Ya Ushindani Wa Kibiashara Katika Maonesho Ya  Biashara
Habari July 5, 2025
Watanzania Watakiwa Kuachana Na Dhana Potofu Kuwa Nishati Safi Ya Kupikia Ni Gharama
Habari July 5, 2025
Wananchi Waelimishwe Kuhusu Utendaji wa Kamati za Maadili za Maofisa wa Mahakama
Habari July 5, 2025
UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili
Habari July 5, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?