MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Vyama Vya Wafanyakazi Vihimize Waajiri Kutoa Taarifa WCF, Zinazohusu Wafanyakazi Wanaopata Ajali, Ugonjwa Kazini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Vyama Vya Wafanyakazi Vihimize Waajiri Kutoa Taarifa WCF, Zinazohusu Wafanyakazi Wanaopata Ajali, Ugonjwa Kazini
Habari

Vyama Vya Wafanyakazi Vihimize Waajiri Kutoa Taarifa WCF, Zinazohusu Wafanyakazi Wanaopata Ajali, Ugonjwa Kazini

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DODOMA: MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umewataka viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini kuwahimiza waajiri kuwasilisha taarifa mapema pindi wafanyakazi wao wanapopata ajali au ugonjwa wakiwa kazini, kuharakisha upatikanaji wa fidia stahiki na kwa wakati ikiwemo fao la matibabu.

Akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Mkurugenzi wa Uendeshaji wa mfuko huo Anselimu Peter amesema fidia zinazotolewa na mfuko huo ni mtiririko wa mafao mbalimbali ikiwemo matibabu ambayo hayana ukomo.

Pia amesema vyama vya wafanyakazi vina haki ya kutoa taarifa WCF kuhusu ajali au ugonjwa unaotokana na kazi endapo mwajiri atashindwa kufanya hivyo.

“Fidia ni mtiririko wa mafao, ambapo fao la kwanza ni la matibabu, sasa mtu akipata ajali au ugonjwa unatokana na kazi tunawaomba nyie muwe chachu ya kuwahimiza waajiri kutoa taarifa mapema katika WCF ili aweze kupata stahiki zake ikiwemo za matibabu.

“Matibabu haya yanaanzia katika hospitali zote ikiwemo Kanda, Taifa na hata Nje ya Nchi,” amesema.

Vile vile amewataka viongozi wa vyama vya wafanyakazi kuwahimiza wafanyakazi wanaopata madhila wakiwa kazini kuwasilisha nyaraka kwa wakati ili Mfuko uweze kufanya tathmini mapema na wahusika walipwe fidia kwa wakati.

Amesema mfuko umechukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa huduma zake zinapatikana kwa njia ya mtandao ili kurahisisha ikiwemo uwasilishaji wa taarifa na nyaraka muhimu.

“Tumeweka mifumo mbalimbali ya kielektroniki ili kurahisisha utoaji wa huduma zetu. Zaidi ya asilimia 90 ya huduma zetu zinapatikana kwa njia ya kielektroniki, ambapo mteja wetu anaweza kupata huduma zetu popote pale alipo,” aliongeza Mha. Peter.

You Might Also Like

Watanzania Wametakiwa Wasiwachague Wanaotumia Rushwa

Ridhiwan Kikwete aitaka LESCO kushirikiana na serikali

Tanzania Kujifunza Teknolojia Ya Magari Ya Umeme Singapore- Biteko

MOI Yaokoa Bilioni 150 Matibabu Ya Kibingwa

Profesa Kabudi Atoa Maagizo Mazito Bodi Ya Ithibati Ya Waandishi Wa Habari

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article PSSSF Yaanza Kulipa Mafao Kwa Kikokotoo  Kipya Kilichoboreshwa – Ridhiwani
Next Article BOT Yafungia Applications 69 Za Mikopo Mtandaoni
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?