MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: WCF yapongezwa kwa Ithibati ya ISO, utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > WCF yapongezwa kwa Ithibati ya ISO, utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa
Habari

WCF yapongezwa kwa Ithibati ya ISO, utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mary Maganga ameuagiza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kuhakikisha inazingatia ubora wa huduma inazotoa kwa wananchi ili kuendana na ithibati ya utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa iliyoupata.
Maganga ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya WCF kukabidhiwa Cheti cha Ithibati ya utoaji wa huduma bora kwa viwango vya kimataifa.
Maganga amesema maboresho yanayofanywa na mfuko huo yanapaswa kuzingatia mahitaji na matarajio ya wateja wake ili kuhakikisha wafanyakazi wanapatiwa haki yao ya fidia stahiki pale wanapopatwa na madhila yatokanayo na kazi zao.
Amesema hayo wakati akikabidhi cheti hicho kwa Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma.
“Kitu cha msingi ni kuhakikisha mnaendelea kuboresha mifumo ya utoaji wa huduma zenu. Nasisitiza mtumie ithibati hii mliyoipata kurahisisha taratibu za kuwasajili waajiri ili ikiwezekana waweze kujisajili wenyewe kwa hiari badala ya kulazimishwa kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria,,” amesema.
Katibu Mkuu huyo ameongeza kuwa jitihada za kutoa elimu kwa wadau wake pamoja na kutumia matokeo ya tafiti mbalimbali ili kuhakikisha huduma zake zinakidhi mahitaji ya wateja ni muhimu kuzingatiwa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. Mduma amesema kuwa mafanikio waliyoyapata yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na uwekezaji mkubwa wanaofanya katika matumizi ya mifumo ya Tehama.
Ametoa rai kwa wadau wa Mfuko huo kutumia huduma za mtandao katika kupata huduma mbalimbali zitolewazo na WCF.
“Tumewekeza katika matumizi ya Tehama, ambapo kwa sasa takribani asilimia 90 ya huduma za Mfuko zinapatikana kwa njia ya mtandao ikiwemo usajili, kutoa taarifa ya madhila kutokana na kazi na kurekebisha taarifa za wafanyakazi.
“Kwa kufanya hivyo tutakuwa tunaoishi maono ya Rais Samia Suluhu Hassan, aliyeelekeza kwamba mifumo ya taasisi zote ni vyema isomane ili kuleta ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi,” amesema.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Viola Masako ameipongeza WCF kwa juhudi kubwa za utendaji hadi kufikia mafanikio hayo yanayoonesha nia thabiti ya Mfuko kuwajibika katika utoaji wa huduma kwa wateja wake kwa viwango vya kimataifa.
“TBS tunaipongeza WCF na tumeshukuru kwa jambo hili kwa sababu linatuongezea wigo wa kuisaidia Serikali yetu kutekeleza majukumu yake kwa wakati na pia kujipima namna ya kuboresha zaidi utoaji wa huduma zake kwa wananchi,” amesema.
WCF ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iliyochini ya Ofisi ya Waziri Mkuu yenye jukumu la kutoa fidia kwa wafanyakazi wanapoumia, kuugua kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao na pale mfanyakazi anapofariki kutokana na kazi wategemezi wa familia yake hulipwa fidia na WCF.

You Might Also Like

Ongezeni Uwajibikaji,Nidhamu, Utendaji Kazi – Bashungwa

Polisi Yatoa Onyo Kali Kwa Waganga wa Tiba Mbadala

Usajili Kwa Njia Ya Mtandao, Umeharakisha Ufunguaji Mashauri

Kamati Ya Bunge Yaridhishwa Na Utaratibu Wa Manunuzi Ya Bando

Huduma ya Mahakama ya Mwanzo yasogezwa Wilaya ya Ubungo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mikataba ya Bilioni 50.9 Yasainiwa kuwezesha nishati safi ya kupikia
Next Article TARI Yawapa Elimu Wakulima, Maofisa Ugani 165 Kilimo Cha Matunda
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

UDSM Yatafiti Ndege Nyuki ‘Drone’ Inayopunguza Uchafuzi Wa Hewa Ukaa
Habari May 29, 2025
Mtafiti UDSM Atafiti Mimea Ya Asili Kudhiti Fangasi Kwenye Mimea
Habari May 29, 2025
Ridhiwani Afanya Mazungumzo Na Balozi Wa China Nchini, Mingjian
Habari May 29, 2025
Kafulila: Deni La Taifa Ni Himilivu
Habari May 29, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?