MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Rais Samia atoa zaidi ya bil. 2.1 usimikaji wa mifumo, uendeshaji mashauri ya wafanyakazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Rais Samia atoa zaidi ya bil. 2.1 usimikaji wa mifumo, uendeshaji mashauri ya wafanyakazi
Habari

Rais Samia atoa zaidi ya bil. 2.1 usimikaji wa mifumo, uendeshaji mashauri ya wafanyakazi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi ya sh bilioni 2.1 kwa ajili ya kuwezesha usimikaji wa mfumo, miundombinu na vitendea kazi, kwa ajili ya uendeshaji na usimamizi wa mashauri  ya wafanyakazi kwa njia ya mtandao.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu,  Protrobas Katambi amesema hayo, alipokuwa akifungua, Mafunzo ya Mfumo wa Uendeshaji na Usimamizi wa Mashauri kwa Njia ya Mtandao (OCMS)  kwa wadau.
“Ninyi wote ni mashahidi kwamba tumemsikia mara nyingi Rais Samia akisisitiza matumizi ya mifumo, na kwamba isomane ili kupunguza na ikibidi kuondoa urasimu katika utoaji wa huduma,”.
Katambi amesema na kuongeza kuwa  utolewaji wa  fedha hizo ni dhahiri amesikia maoni ya wafanyakazi yaliyotolewa siku kuu ya wafanyakazi (Mei Mosi).
Amesema mifumo hii itawafanya wananchi waweze kupata taarifa na kuhudumiwa kwa muda mfupi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi ( CMA), Usekelege Mpulla amesema, wakati wa Maadhimisho ya Mei Mosi Kitaifa mwaka huu, upande wa wadau hususan waajiri na waajiriwa waliwasilisha hoja kuhusu mifumo ya utatuzi ya migogoro ya kazi nchini.
Amesema,” Na hoja kubwa ilikuwa ni Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, huduma zake hazipo kila mahali, serikali sikivu baada ya kusikia hilo, ilijibu kwa kuwasilisha na kuelezea kuhusu mkakati huu, ambao Rais Samia ndani ya muda mfupi ametenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba unatekelezeka,”.
Amesema mfumo huo ukianza kutumika utakuwa ni majibu kwa changamoto za muda mrefu za wananchi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Mpulla amesema, kabla ya kuanza kwa matumizi ya mfumo huo, tangu kuanzishwa kwa tume ya usuluhishi na uamuzi mwaka 2007, tume ilitatua migogoro ‘manual’.
“Tulikuwa tunatakiwa kupeleka majalada Mahakama Kuu na kumekuwa na malalamiko ya uchelewaji.
“Mfumo huu mpya, taarifa zake zitasomana na mahakama, zitasomana na Ofisi ya Kamishna wa Kazi kwa wafanyakazi ambao ni wageni wanaopata vibali kufanya kazi nchini,” amesema.
Pia amesema kupitia mfumo huo, wadau mbalimbali wataweza kuwasilisha mashauri bila ya kupanga foleni kwenye tume ya usuluhishi na uamuzi, ama kusafiri umbali mrefu.
Amesisitiza pia, kupitia mfumo huu, ufanisi katika tume hiyo utaongezeka, pia utatuzi wa migogoro ya kikazi utakwenda kwa haraka zaidi ya ilivyozoeleka.

You Might Also Like

Gridi Ya Taifa Ni Dhaifu Kwa Mikoa Ya Kaskazini-Mramba

Watafiti Wa Mimea Vamizi Watua Serengeti

SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele

Rais Samia azindua bwawa la umwagiliaji Mtibwa

Kamati Ya Bunge  Yaridhishwa Na Ujenzi Wa Jengo La Kituo Cha Zimamoto, Mtumba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Kuendelea Kutenga Fedha Kwa ajili ya Ukamilishaji wa Maboma ya Vituo vya Afya
Next Article Apongeza watumishi kwa kutoa huduma bora kwa walimu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

PSPTB Yatangaza Usajili wa Mitihani ya 31 ya Kitaaluma ya Ununuzi na Ugavi
Habari July 4, 2025
TARI Yatikisa Sabasaba Na Mti Wa ‘Allspice’
Habari July 4, 2025
TMDA Kudhibiti Bidhaa Za Tumbaku Ili Wananchi Wasiendelee Kupata Madhara
Habari July 4, 2025
Rais Dk Mwinyi Kukata Keki Sabasaba
Habari July 4, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?