MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Watanzania lindeni Viwanda vya Ndani
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Watanzania lindeni Viwanda vya Ndani
Habari

Watanzania lindeni Viwanda vya Ndani

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu
WATANZANIA wametakiwa kulinda viwanda vya ndani ya nchi pamoja na kutumia bidhaa zinazotengenezwa humo ili kuviwezesha kuendelea na uzalishaji, kuongeza ajira, na kukuza uchumi kwa ujumla.

Waziri wa. Viwanda na Biashara, Dk Selemani Jafo amesema hayo akiwa ziarani mkoa wa Kilimanjaro na kuwataka Watanzania kulinda viwanda vya Serikalli kwa kufanya kazi kwa uadilifu, weledi, uzalendo na hofu ya Mungu ili kiepuka kusababisha uharibifu unaoweza kutokea.

Amesema Serikali imewekeza fedha nyingi kuvifufua viwanda hivyo na kuviendesha .

Akiwa katika ziara hiyo ametembelea viwanda, kuongea na Wafanyabiara pamoja na Maofisa Biashara wa Mkoa huo kwa lengo la kujionea shughjuli za uzalishaji, kusikiliza changamoto na kuona njia bora ya kuzitatua kwa kushirikiana na taasisi nyingine .

Aidha, Waziri Jafo akiwa mkoani humo ametembelea Kiwanda cha Kutengeneza Vinywaji baridi cha Kiwanda cha A One product and Bottles Ltd, Kiwanda cha Bonite Bottlers Ltd, Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi cha Kilimanjaro, Kiwanda cha kutengeneza vipuri na mitambo mbalimbali cha KMTC, Eneo la uwekezaji la bustani ya wanyamapori ya Serval (Serval Wildlife) pamoja na Kiwanda cha Sukari Moshi (TPC).

Akiwa katika Eneo la uwekezaji la bustani ya wanyamapori ya Serval (Serval Wildlife) Dkt. Jafo amewahimiza Watanzania kutumia muda wao wa mapumziko kufanya utalii wa ndani ili kukuza biashara ya utalii na kuvutia wafanyabiashara katika sekta hiyo.

Katika hatua nyingine akiongea na Wafanyabiashara na Wamiliki wa Viwanda wa Mkoa wa Kilimanjaro, Waziri Jafo amewataka Watumishi wa Umma Mkoani humo kiwasaidia wafanyabiashara na amewaahidi kuwa atashirikiana na Taasisi nyingine za kisekta kutatua changamoto zilizopo kwa lengo la kuendelea kuweka mazingira bora ya biashara.

Vilevile Dkt Jafo amehamasisha utekelezaji wa Mpango wa Viwanda Tqnzania unaoelekeza kuwa kila Mkoa unapaswa kuanzisha Viwanda vikubwa vitatu, Viwanda vya kati vitano , Viwanda vidogo 20 na Viwanda vidogo sana 30 ili kukukuza sekta ya viwanda kuongeza ajira na pato la Taifa

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa Wilaya ya Rombo Raymod Mwangala ameahidi kwa Mkoa wa Kilimanjaro utaendelea kufufua viwanda vya zamani visivyofanya kazi na kuanzisha vipya ili kiongeza ajira na pato la taifa mkoani humo.

You Might Also Like

Ujenzi Miundombinu ya Kuongeza Udahili kipaumbele Cha Serikali

Masoko mapya nje ya nchi kuipatia nchi sh. trilioni 10

Wasilisheni Migogoro Yenu Tume ya Usuluhishi na Uamuzi – Massawe

Limeni mkonge unalipa – Maghali

RAAWU yapokea migogoro 16, yaishughulikia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article GIZ, IUCEA waratibu uchambuzi wa data kidijitali kwa wahitimu
Next Article Watumishi wa Umma wafahamu haki ya rufaa Kwa mujibu wa sheria
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?