MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wadau wa uchukuzi zingatieni maslahi ya wafanyakazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wadau wa uchukuzi zingatieni maslahi ya wafanyakazi
Habari

Wadau wa uchukuzi zingatieni maslahi ya wafanyakazi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Lyatuu
DAR ES SALAAM: SERIKALI imewataka wadau wa usafirishaji  kuzingatia maslahi ya wafamyakazi wao kwani yapo malalamiko kutoka Kwa wafanyakazi kutotendewa haki.
Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile amesema hayo  Dar es Salaam katika jukwaa lililoandaliwa na Taasis ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili pamoja na kuzitafutia suluhisho.
Akizungumza baada ya kusikiliza changamoto za Sekta hiyo, Kihenzile amesema pamoja na mambo mengine lakini wadau hao wajitahidi kutenda haki kwa wafanyakazi wao ikiwa ni pamoja  na kuwalipa inavyostahili.
Kumbukeni kuwepo kwenye hizo nafasi ni Kwa neema ya Mungu tu..watendeeni vyema mkijua kuwa yapo malipo mbele ya haki,” amesema Kihenzile na kuwataka pia kutambua mageuzi ya uboreshaji wa sekta hiyo yanayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Kuhusu mageuzi Kwa sekta hiyo amesema ni Vizuri kuelewa nchi inakoelekea,na kujipanga namna ya kufikia fursa zilizopo katika sekta hiyo.
Kihenzile amesema eneo lingine linaloangaliwa Kwa maboresho ni kwenye kujenga bandari kavu katika eneo la Tunduma ambapo tayari imemepata ekari 6000 lengo kuondoa msongamano wa malori ya mizigo.
Hata hivyo alitoa wito kwa taasisi za fedha kushusha riba na kuwakopesha wadau wa sekta  hiyo Ili kuzifikia fursa mbalimbali lengo likiwa ni kukuza uchumi na hata kuongeza ajira.
Awali akizungumza Mtendaji Mkuu wa TPSF,  Rafael Maganga amesema taasisi hiyo inaadhimisha  miaka 25 tangu kuanzishwa ikiwa na lengo  kukuza uchumi kufika dira ya maendeleo 2050.
Amesema kongamano limewaleta pamoja  wadau mbalimbali wa maendeleo Ili kujadili changamoto zinazoathiri ufanisi wa sekta hiyo na kuwataka kutoa mapendekezo yao.
“Michango wa sekta unakuwa Kwa asilimia nane na inaumganisha  sekta zote nchini,hivyo changamoto zilizopo ziweze kufanyiwa kazi,” amesema.

You Might Also Like

VETA Yafanya Mageuzi Makubwa Yaliyowezesha Wengi Kuajiriwa

Tunatekeleza Azma YA Rais Samia Kuwafikia Wananchi Waliojiajiri

JOWUTA Yakutana na Waziri Ridhiwani, Kamishna wa Kazi Kujadili Changamoto za Wanahabari

Ridhiwani Aiagiza CMA Kushughulikia Migogoro Kwa Haraka, Ufanisi

Wafugaji huchakachua maziwa kwa kuongeza mafuta, maji, magadi au mkojo wa ng’ombe

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa
Next Article Wajadili uendelezaji mazao ya utalii
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?