Na Lucy Lyatuu
SHIRIKA La Uzalishaji Mali La Jeshi La Polisi Tanzania limeeleza kuwa na.mkakati wa lazima wa ukaguzi wa vyombo vya moto.mradi ambao ni mkubwa ukihusisha kujenga vituo vya ukaguzi wa vyombo vya moto vya kisasa nchi nzima.
Ofisa Uhusiano wa Shirika hilo,Mrakibu Msaidizi wa Polisi Lule Mlay amesema hayo wakati akizungumza katika banda la shirika hilo lililoko katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Dar es Salaam na kuongeza kuwa ni mara ya kwanza kwa Shirika hilo kushiriki maonesho ya biashara ya 50 ya kimataifa maarufu kama sabasaba kwa ajili ya kuonesha miradi mbalimbali inayotekelezwa.

Amesema mradi mwingine wa kimkakati utakaotarajiwa kuanza ni wa miji salama ambapo shirikanlitashirikiana na serikali kujenga kamera za kisasa kwenye miji mikubwa mitatu ambayo ni Arusha,Dar es Salàm na Dodoma ili kukabiliana na vitendo vya kihalifu.
Amesema lakini pia shirika lina mradi wa kimkakati wa kufunga kamera za kiusalama kwenye barabara kuu ambapk itashirikiana na Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani ili kuangalia wanaofanya makosa ya uvunjifu wa sheria ya usalama barabarani.
“Kwa kuanzia zitajengwa kamera kuanzia daraja la John Kijazi Interchange mpaka Dodoma,” amesema na kuongeza kuwa mradi mwingine ni wa ushonaji wa nguo,ambapo shirika linashona sare za kampuni za serikali pamoja na kampuni ninafsi zikiwemo za ulinzi.

“Kwa sasa tunafanya kazi na wenzetu Polisi Wasaidizi wa Chuo Kikuu chabDarnes Salam lakini tunafanya kazi na Jeshinla Magereza,Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),” amesema na kuongeza mradi mwingine ni kupitia kampuni ya ulknzinyabJeshi la Polisi (URA) kutoa huduma ya ulinzi
Mlay amesema kwa sasa wanalinda Shirikanla Masoko la Kariakoo Dar es Salaam pia kagika vituo vyote vya mwendokasi DART,pia katika maonesho hayo ya sabasaba wanafanya kazi.

Kwa upande wake Koplo Issa Godwin amesema katika maonesho hayo wamekuja kuonesha mradi wa shirika wa kutoa mafunzo kwa kampuni za ulinzi binafsi,mafunzo sahihi ya silaha lakini mradi mwingine ni wa huduma za kibandari.
“Ieleweke kuwa asilimia 60 ya wafanyakazi wa bandari ni wa kutwa hivyo mi muhimu kupata huduma,” amesema na kuongeza kywa kuna mradi wa usafirishajibwa fedha na vitu vya thamani na kuwataka watanzania kutumia shirika hilo kwa huduma mbalimbali.


