MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ruhuka: Mdudu Anayetishia Zao la Kahawa, TARI Yaja na Suluhisho
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ruhuka: Mdudu Anayetishia Zao la Kahawa, TARI Yaja na Suluhisho
Habari

Ruhuka: Mdudu Anayetishia Zao la Kahawa, TARI Yaja na Suluhisho

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
KAHAWA ni miongoni mwa mazao ya biashara yanayochangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa Tanzania kupitia mauzo ya nje na kipato cha wakulima.
Hata hivyo, mafanikio ya zao hilo yanaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali, mojawapo ikiwa ni mashambulizi ya wadudu waharibifu.
Habari Picha 12711
Miongoni mwa wadudu hao, ruhuka ametajwa kuwa adui mkubwa wa zao la kahawa duniani.
Kwa mujibu wa Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kupitia Kituo cha Utafiti wa Kahawa cha TaCRI Lyamungu, Dkt. Godsteven Maro, ruhuka ni mdudu anayeshambulia punje za kahawa kwa kutoboa matunda na kuingia ndani ya punje.
Kitendo hicho huharibu ubora wa kahawa na kupunguza thamani yake sokoni, hivyo kuwaingizia wakulima hasara kubwa.
Dkt. Maro anazungumza hayo katika Maonesho ya 50 ya Sabasaba yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.
Anasema mdudu huyo si tatizo la Tanzania pekee, bali ni changamoto inayowakabili wazalishaji wa kahawa duniani.
Nchi kama Colombia zimekuwa zikiwekeza katika tafiti za kudhibiti ruhuka kwa kutumia mitego maalumu ya kumvutia na kumtega.
Kutokana na uzoefu huo, watafiti wa TaCRI wameboresha teknolojia hiyo ili iendane na mazingira ya Tanzania.
Mtego huo umetengenezwa kwa kutumia vifaa vinavyopatikana kwa urahisi, huku ukitumia vimiminika kama spiriti au pombe za kienyeji kuvutia wadudu hao.
Kwa mujibu wa watafiti, mtego mmoja unaweza kunasa hadi wadudu ruhuka 600 kwa kipindi cha wiki moja.
Hii inaonyesha kuwa teknolojia hiyo inaweza kupunguza kwa kiwango kikubwa idadi ya wadudu wanaoshambulia mashamba ya kahawa ikiwa wakulima wataitumia kwa usahihi.
Faida nyingine ya mtego huo ni kwamba ni wa gharama nafuu na unaweza kutengenezwa na mkulima mwenyewe bila kuhitaji vifaa vya gharama kubwa.
Hali hiyo inaufanya kuwa suluhisho linalofaa kwa wakulima wadogo na wakubwa.
Kwa sasa, ruhuka ameendelea kuongezeka katika mashamba ya kahawa aina ya Arabica na Robusta nchini Tanzania.
Wataalamu wanaonya kuwa bila kuchukua hatua za haraka, mdudu huyo anaweza kuendelea kupunguza uzalishaji na ubora wa kahawa ya Tanzania.
Dalili za mashambulizi ya ruhuka ni pamoja na kuwepo kwa tundu moja au zaidi kwenye kitovu cha tunda la kahawa, iwe tunda bado ni bichi au limeiva.
Wakulima wanashauriwa kukagua mashamba yao mara kwa mara ili kubaini dalili hizo mapema na kuanza kutumia mbinu za udhibiti kabla uharibifu haujaongezeka.
Mbali na matumizi ya mitego, wataalamu wanasisitiza umuhimu wa kutumia mbinu za udhibiti husishi wa wadudu, ikiwa ni pamoja na usafi wa shamba, kuvuna kwa wakati, kuondoa matunda yaliyoshambuliwa na kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo.
Kadiri sekta ya kahawa inavyoendelea kuwa nguzo muhimu ya uchumi wa Tanzania, matumizi ya teknolojia rahisi na bunifu kama huu wa TaCRI yanaweza kuwa suluhisho muhimu katika kupunguza hasara zinazotokana na wadudu waharibifu na kuongeza uzalishaji wa kahawa yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko la dunia.

You Might Also Like

VETA Yawasilisha Teknolojia ya Hybrid Katika Maadhimisho ya Wiki ya Vijana

Ubunifu Wa Majengo Watakiwa Kuzingatia Tija Na Gharama Nafuu

Rais Mpya CWT Ikomba: ‘Nataka Kuwaunganisha Walimu, Kuitendea Haki Kazi Yetu’

Polisi Kuimarisha Ulinzi Nyumba Za Ibada Krismasi, Mwaka Mpya

Waziri Mkuu Majaliwa Ahimiza Watanzania Kufanya Mazoezi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article BRELA Yaja Na Mfumo BOS Uliounganisha Mifumo Yote
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

BRELA Yaja Na Mfumo BOS Uliounganisha Mifumo Yote
Habari July 12, 2026
Misitu Ni Moyo Wa Maendeleo Endelevu-TFS
Habari July 12, 2026
Profesa Nagu Aridhishwa Na Huduma Katika Banda Jumuishi La Ofisi Ya Waziri Mkuu Sabasaba 
Habari July 12, 2026
JAB Yazindua Mwongozo Wa Kisheria Wa Utoaji Ithibati Ya Maisha Kwa Wanahabari Wakongwe
Habari July 12, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?