MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Askofu Chilongani Aitaka Jamii Kutumia Ijumaa Kuu Kusameheana na Kujenga Umoja
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Askofu Chilongani Aitaka Jamii Kutumia Ijumaa Kuu Kusameheana na Kujenga Umoja
Habari

Askofu Chilongani Aitaka Jamii Kutumia Ijumaa Kuu Kusameheana na Kujenga Umoja

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi wetu
DODOMA: ASKOFU wa Kanisa Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Central Tanganyika, Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu, Dkt. Dikson Chilongani, ameitaka Serikali na Watanzania kwa ujumla kuitumia siku ya Ijumaa Kuu kama fursa ya kusameheana na kuacha nyuma changamoto zilizopita.
Akizungumza Aprili 3, 2026, katika ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika kanisani hapo, Askofu Chilongani amesema siku hiyo, inayokumbuka mateso na kifo cha Yesu Kristo, inapaswa kuwa chachu ya upendo, umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.
Amesisitiza kuwa viongozi wa Serikali na wa dini wanapaswa kutumia nafasi zao kuimarisha umoja wa kitaifa kwa kuondoa chuki, ubinafsi na migawanyiko isiyo na tija.
Habari Picha 11676
Amebainisha kuwa ni muhimu kwa viongozi hao kuonesha mfano kwa kusameheana na kuweka mazingira yatakayowezesha wananchi kuishi kwa amani.
“Tumepitia changamoto mbalimbali katika kipindi kilichopita, hivyo ni wakati wa kuziachilia na kuanza ukurasa mpya wa upendo na mshikamano kwa ajili ya ustawi wa taifa,” amesema.
Aidha, Askofu Chilongani ameeleza kuwa msamaha si wa viongozi pekee, bali ni jukumu la kila Mtanzania, kwani ni tendo la kiroho linalochangia kujenga jamii yenye maelewano na utulivu.
Katika mahubiri hayo, ameongeza kuwa taifa lenye afya linahitaji viongozi na wananchi wanaojali, wanaosikilizana na wanaoepuka chuki pamoja na ubinafsi.
Wakati huo huo, Mchungaji Adrian Mdao, akisoma somo la tano kati ya masomo saba, amesisitiza umuhimu wa kusikiliza sauti za wenye uhitaji.
Amesema baadhi ya wazazi na watumishi wa umma wamekuwa wakipuuza wajibu huo kutokana na majukumu au kutokuwa tayari kusikiliza changamoto za wengine.
Habari Picha 11677
Ametoa wito kwa walio na mamlaka kutumia nafasi zao kusaidia badala ya kuumiza, akisisitiza kuwa kusikiliza na kujibu mahitaji ya watu ni msingi wa kujenga jamii yenye upendo, kuaminiana na mshikamano.

You Might Also Like

TALGWU Chafanya Kikao Cha Baraza La Wafanyakazi Dodoma

Wambali: Vyama Vya Wafanyakazi Muhimili wa Uchumi, Ustawi Wa Jamii

Madiwani  Saidieni Wananchi Njia Sahihi Ya  Kutoa Taarifa Za Hitilafu Za Umeme-Mpogolo

Dkt. Adesina Wa AfD Avutiwa Na Mwenendo Uchumi Wa Tanzania

Hivi Ndivyo Vipaumbele Vya Maliasili

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TAWIA na MAIPAC washirikiana kuadhimisha Siku ya Wajane, wapanga kupanda Mlima Kilimanjaro
Next Article Serikali Yaanza Mikakati Ya Kukabiliana Na Wanyamapori Wakali, Waharibifu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Kanisa Laitaka Serikali Kuchukua Hatua Dhidi ya Rushwa
Habari April 5, 2026
CWT Yashauri Walimu Wasiwe Wasimamizi Wa Miradi
Habari April 4, 2026
Serikali Yaanza Mikakati Ya Kukabiliana Na Wanyamapori Wakali, Waharibifu
Habari April 4, 2026
TAWIA na MAIPAC washirikiana kuadhimisha Siku ya Wajane, wapanga kupanda Mlima Kilimanjaro
Habari April 4, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?