MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Habari

Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy Lyatuu

WAZIRI  wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amezindua mita Janja (Smart Meters) za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), zinazotumia mfumo mpya wa kisasa  na kuagiza zisambazwe nchi nzima na wateja wapya wafungiwe mita hizo.

 

Amesemamita hizi zina mfumo unaolenga kuboresha utoaji wa huduma za umeme nchini na kuongeza ufanisi kwa Shirika na wateja wake.

Akizungumza katika hafla hiyo  Ndejembi ametoa pongezi  kwa  TANESCO kwa hatua kubwa ya kimapinduzi waliyoifikia katika maboresho ya huduma kwa umma.

Ameiagiza Tanesco kuanzisha  mfumo   utakaorahisha muingiliano kati ya Shirika na wateja wake ikiwa ni mwendelezo wa kuendana na kasi na mapinduzi ya teknolojia ya sasa.

Habari Picha 10517

 

Kadhalika ameishauri Tanesco kuendelea kuboresha mawasiliano ya mara kwa mara na wateja ili kuimarisha utoaji huduma wa kisasa.

 

“Uzinduzi wa Mita Janja hizi ni uthibitisho wa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia , kuhakikisha wananchi wanapata umeme bora, wa uhakika na unaoendana na mabadiliko ya teknolojia ya kisasa,” amesema.

Waziri Ndejembi amekumbusha changamoto ambazo wateja walikuwa wanakutana nazo kwa kutumia mita za zamani, ikiwemo kushindwa kuona matumizi ya umeme kwa wakati halisi, ugumu wa kupanga bajeti, pamoja na hitilafu mbalimbali kama tokeni kushindwa kuingia, kupotea kwa kumbukumbu au kuharibika kwa rimoti za kuingiza tokeni.

Habari Picha 10518

Ameeleza kuwa baadhi ya mita zilikwekwa katika maeneo magumu kufikika, hali iliyowalazimu wateja kupanda ngazi au stuli kila wanaponunua umeme, jambo lililosababisha usumbufu mkubwa hasa wakati wa dharura.

Ameeleza kuwa kuanzishwa kwa Mita Janja ni matokeo ya uamuzi wa Serikali na TANESCO kupambana na changamoto hizo kwa kutumia teknolojia ya kisasa.

Amesema kupitia mita hizo mpya, wananchi wataweza, kuingiza umeme popote walipo bila kulazimika kufika nyumbani,kufuatilia matumizi yao kwa muda halisi kupitia mfumo mahiri na kupata taarifa za kuisha kwa umeme kwa wakati kupitia kiashiria (alert).

Amesema mita hizo zitasaidia kubaini wizi wa umeme, kutambua uharibifu wa mita, na kupunguza upotevu wa nishati kwa wakati halisi, hivyo kuimarisha mapato ya shirika na kulinda fedha za Serikali.

Habari Picha 10519

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Lazaro Twange amesema mita hizo zinafaida ikiwemo kutunza kumbukumbu kwa muda mrefu, zina suluhisho endapo mteja akinunua umeme kwa bahati mbaya.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba amesema sekta ya nishati inakuwa kwa teknolojia  kwa kiwango kikubwa.

Habari Picha 10520

 

 

You Might Also Like

Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi

Italia Kuangazia Fursa Za Uwekezaji Ambazo Hazijatambuliwa

Kanisa La GCC Kufanya Maombi Kuelekea Uchaguzi Mkuu

Miradi Dodoma Yamkuna Rais Samia

Ntonda Ameipongeza TEA Kwa Utekelezaji Bora Wa Miradi Ya Elimu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Habari December 5, 2025
Msama Aipongeza Hotuba Ya Samia, Atoa Neno Kwa Vijana, Wazee, Wanaharakati
Habari December 4, 2025
Profesa Silayo Aaga, Jawara Kuchukua Uongozi Mpya wa AFWC25
Habari December 3, 2025
Mpango Wa Taifa Wa Teknolojia Uko Mbioni Kuja-Serikali
Habari December 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?