MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Madiwani  Saidieni Wananchi Njia Sahihi Ya  Kutoa Taarifa Za Hitilafu Za Umeme-Mpogolo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Madiwani  Saidieni Wananchi Njia Sahihi Ya  Kutoa Taarifa Za Hitilafu Za Umeme-Mpogolo
Habari

Madiwani  Saidieni Wananchi Njia Sahihi Ya  Kutoa Taarifa Za Hitilafu Za Umeme-Mpogolo

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Lucy  Lyatuu

MADIWANI na Wenyeviti wa serikali  za mitaa ya Ilala, Temeke na Kigamboni, Dar es Salaam wamehimizwa kuwasaidia wananchi kufahamu hatua sahihi za kutoa taarifa za hitilafu za umeme kupitia mfumo mpya wa Nihudumie, ambao unatoa huduma kwa haraka na bila gharama.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo ametoa rai hiyo Dar es Salaam wakati akifungua kikao kazi kilichoandaliwa na (TANESCO) kwa ajili ya kuwakutanisha viongozi hao.

Amewataka viongozi hao kushirikiana kikamilifu na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ili kuwezesha utoaji wa huduma bora na ya uhakika ya umeme kwa wananchi.

Amesema  sifa ya kiongozi bora ni kuishi na kutatua changamoto za wananchi, ikiwemo hitaji la umeme wa uhakika na kuwasihi kuendelea kushirikiana na Tanesco ili kuhakikisha changamoto za upatikanaji wa umeme zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Habari Picha 10382

Amesema serikali inatambua na kuthamini ushirikiano unaoendelea kati ya viongozi wa serikali za mitaa na TANESCO, katika kuhakikisha huduma za umeme zinawafikia wananchi kwa wakati na kwa ufanisi.

 

Kuhusu huduma ya umeme, amesema viongozi wa serikali za mitaa wana nafasi ya kipekee katika kusimamia masuala ya umeme kwa kuwa wao ndio wapo karibu na wananchi.

 

Mpogolo amesisitiza umuhimu wa viongozi kusimamia ulinzi wa miundombinu ya umeme, ikiwemo nguzo na nyaya, hasa katika maeneo ya mijini ambayo yanakabiliwa na uharibifu kutokana na shughuli za ujenzi ambapo baadhi ya uharibifu huo husababishwa na watu wanaounganisha umeme kiholela, jambo linalosababisha madhara kwa jamii.

 

Amewataka viongozi wa wilaya na TANESCO kuendeleza mafunzo kama hayo katika maeneo mengine ya jiji ili kuongeza uelewa na kuboresha mahusiano baina ya viongozi na shirika hilo  huku akiwashukuru waliojitokeza licha ya majukumu yao mengi.

 

“Kutenga muda wa kushiriki mafunzo haya ni ishara ya kujitoa katika kuhudumia wananchi, jambo ambalo limewezesha TANESCO kutekeleza dhamira yake ya kutoa elimu na kupokea changamoto zinazowakabili wananchi kwenye maeneo yao,’amesema.

 

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Irene Gowele, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO LazaroTwange, amesema TANESCO imeanzisha mkakati wa kushirikiana kwa karibu na viongozi wa mitaa ili kuboresha upatikanaji wa taarifa, kuharakisha huduma na kutatua changamoto za umeme kwa ufanisi zaidi.

Amesema kupitia mafunzo na majadiliano yao, viongozi hao wataelezwa miradi ya kimkakati inayoendelea katika maeneo yao na namna wanavyoweza kuwa daraja la mawasiliano kati ya wananchi na shirika.

 

Aidha, amebainisha kuwa serikali kwa sasa inaelekeza nguvu katika kuwahudumia wananchi moja kwa moja, na hivyo ushirikiano na viongozi wa mitaa ni muhimu.

 

You Might Also Like

Dkt. Mashimba Achukua Fomu Ya Kuwania Nafasi Ya Ubunge

Dar Sasa Kufanya Biashara Saa 24, Kuanza Februari 22 Mwaka Huu

OUT Yawapiga Msasa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa

Ndege Ya TPHPA Yatua Rasmi Kudhibiti, Kwelea Kwelea, Viwavijeshi, Nzige 

MSD Yaokoa Zaidi Ya Mil. 15

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Rais Samia Awateua Tido Mhando, Machumu Na Nyalandu
Next Article Jamii Yaaswa Kujenga Utamaduni wa Kusoma Vitabu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?