MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: ICGLR Yajipanga Kujiimarisha Amani Katika Kanda
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > ICGLR Yajipanga Kujiimarisha Amani Katika Kanda
Habari

ICGLR Yajipanga Kujiimarisha Amani Katika Kanda

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
JUMUIYA ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) imetajwa kuwa jukwaa muafaka la kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa changamoto zinazozikabili nchi wanachama, hususan matatizo ya ukosefu wa amani, usalama na maendeleo endelevu.
Kauli hiyo imetolewa mjini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Novemba 13 , 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa Mawaziri wa ICGLR uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa DRC, Judith Tuluka Suminwa.
Habari Picha 10313
Katika mkutano huo, nchi wanachama zimetakiwa kuenzi na kutekeleza kwa dhati Mkataba wa kuanzishwa kwa Jumuiya hiyo, ambao unalenga kupatikana kwa amani, usalama na maendeleo ya kweli kupitia umoja, ushirikiano na mshikamano, sambamba na kujitoa kwa hali na mali katika kufikia malengo hayo.
Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa. Tanzania imeunga mkono ajenda zinazojadiliwa, hususan zile zinazohusu amani na usalama, na imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kuchangia juhudi za kurejesha na kudumisha amani katika Kanda.
Habari Picha 10314
Akizungumza wakati wa ufunguzi, Waziri Mkuu wa DRC amebainisha kuwa nchi za ICGLR bado hazijafikia malengo ya msingi ya Mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya hiyo—ambayo ni amani, usalama na maendeleo.
Ametoa wito kwa nchi wanachama kuongeza umoja, mshikamano na ushirikiano ili kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa changamoto za kiusalama. Aidha, alitaja ukosefu wa rasilimali fedha na miundombinu duni ndani na baina ya nchi wanachama kama sababu zinazochangia kutofikiwa kwa malengo hayo.
Katika hitimisho la hotuba zao, viongozi walisisitiza umuhimu wa nchi za ICGLR kubuni mikakati ya ndani ya kukabiliana na changamoto zinazoikabili Kanda bila kutegemea msaada wa nje. Pia walihimiza kuimarishwa kwa taasisi za kikanda kwa kuzitengea rasilimali fedha na wataalamu ili ziweze kushughulikia kikamilifu changamoto za amani na usalama.
Habari Picha 10315
Habari Picha 10316
Habari Picha 10317

You Might Also Like

NIC Yatoa Elimu ya Bima Kwenye Kijiji cha Bima, Maonesho ya Madini Geita

Atoa Maelekezo Kwa Chuo Cha Hombolo Kuwajengea Uwezo Viongozi Wa Mitaa Na Vijiji -Kapinga

Ridhiwani: WCF Umeboresha Mifumo Ya Ushughulikiaji Wa Fidia

Tutumie Mitandao Kwa Matumizi Yenye Manufaa – Kilimbe

Mbunge wa Monduli Aahidi Kusimamia Changamoto za Jimbo Lake

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kigae: Mwigulu Waziri Mkuu Mahiri
Next Article Rais Samia Amwonya Mwigulu Dhidi Ya Vishawishi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?