MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Dkt Natu Mwamba Ashuhudia Utiaji Saini CRDB Na Taasisi Tatu Za Fedha Kimataifa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Dkt Natu Mwamba Ashuhudia Utiaji Saini CRDB Na Taasisi Tatu Za Fedha Kimataifa
Habari

Dkt Natu Mwamba Ashuhudia Utiaji Saini CRDB Na Taasisi Tatu Za Fedha Kimataifa

Author
By Author
Share
3 Min Read

Na Mwandishi Wetu

KATIBU  Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, ameshuhudia tukio la Benki ya CRDB ikisaini  ubia mkubwa wa kimkakati na taasisi tatu za fedha za kimataifa wenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 300, kwa ajili ya kuendeleza ujumuishwaji wa fedha na maendeleo endelevu barani Afrika, tukio lililofanyika jijini Washington D.C., nchini Marekani.

 

Benki ya CRDB imeingia katika ushirikiano huo na FinDev Canada, DEG (KfW Group, Ujerumani), na Shelter Afrique Development Bank (ShafDB), ikiwa ni hatua muhimu katika safari ya benki hiyo ya kuendeleza ujumuishwaji wa fedha na maendeleo endelevu barani Afrika.

Habari Picha 10089

 

Hati za Makubaliano (MoUs) zilisainiwa wakati wa Jukwaa la Wabia na Wawekezaji  “Investors and Partners Forum” lililofanyika kando ya Mikutano ya Mwaka ya Benki ya Dunia na IMF jijini Washington D.C.

 

Jukwaa hilo la kimataifa lililoandaliwa na Benki ya CRDB lilikutanisha wawekezaji wa kimataifa na viongozi wakuu wa serikali kutoka Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

 

Viongozi mbalimbali wa kimataifa walishiriki jukwaa hilo ikiwemo Waziri wa Fedha wa Burundi, Waziri wa Habari wa DRC, Magavana wa Benki Kuu za Tanzania na Burundi, Mabalozi wa Tanzania na Burundi nchini Marekani, pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha ya Tanzania, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, ambaye aliongoza ujumbe wa Tanzania katika Mikutano ya Benki ya Dunia na IMF na ambae pia alikuwa Mgeni Rasmi katika jukwaa hilo.

 

Makubaliano hayo yamesainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, pamoja na viongozi wakuu wa taasisi washirika: Mkurugenzi Mtendaji wa Shelter Afrique Development Bank Thierno-Habib Hann, Mkurugenzi Mtendaji wa DEG Roland Siller, na Mkurugenzi Mtendaji wa FinDev Canada Lori Kerr.

Habari Picha 10090

 

Ukuaji Jumuishi: Kupitia ushirikiano na FinDev Canada, Benki ya CRDB imepata uwezeshwaji wa Dola za Kimarekeni Milioni 60 zinazolenga kupanua mikopo kwa wajasiriamali wachanga, wadogo, na wa kati (MSMEs), kukiwa na msisitizo maalum kwenye biashara zinazoendeshwa na wanawake na miradi inayohimili mabadiliko ya tabianchi.

 

Uwezeshaji wa Biashara Ndogo na za Kati (SME): Kupitia DEG, Benki ya CRDB itatoa Dola za Kimarekani Milioni 50 kwa ajili ya mikopo midogo midogo ya biashara ndogo na za kati (SME), kusaidia ukuaji wa biashara, ubunifu, na uzalishwaji wa ajira nchini Tanzania.

 

Kuhusu  Usawa wa Kijamii na Makazi Nafuu, Ushirikiano na Shelter Afrique Development Bank unalenga kupunguza upungufu wa makazi katika kanda, ambapo kwa kuanzia Benki ya CRDB imepokea Dola za Kimarekani Milioni 10 kwa ajili ya kampuni tanzu yake ya nchini DRC.

Habari Picha 10091

 

Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, DKT. Natu El-maamry Mwamba, ametoa wito kwa jumuiya ya Kimataifa kwewekeza mitaji na teknolojia nchi Tanzania kutokana na fursa mbalimbali zilizomo ikiwemo soko la uhakika la biashara, sera nzuri na vivutio mbalimbali vya uwekezaji.

You Might Also Like

Sagini Amwelezea Kaluta Amir Abeid Ni Alama Ya Kuigwa

Msomi Wa Afya, Fatuma Atia Nia Jimbo la Dodoma Mjini

Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi

CHAUMMA Yataka Kuvunja Bodi ya Korosho, Kuunda Mamlaka Mpya ya Mazao ya Kimkakati

Taasisi Za Serikali Zapewa Wiki Tano Kujiunga Na Mfumo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tanzania Na Africa50 Wazidi Kuimarisha Ushirikiano
Next Article Matukio Mbalimbali Ya Kampeni Za CCM Dar
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Matukio Mbalimbali Ya Kampeni Za CCM Dar
Habari October 21, 2025
Tanzania Na Africa50 Wazidi Kuimarisha Ushirikiano
Habari October 21, 2025
Madaktari Kutoka Ireland Watoa Matibabu Ya Mifupa Kwa Watoto MOI
Habari October 20, 2025
Mwalim: Nikichaguliwa urais, Kigaila atakuwa Waziri Mkuu wangu
Habari October 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?