MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yapeleka Sh Bil 10 Kwa Kiwanda Cha Viuadudu Cha TBPL
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yapeleka Sh Bil 10 Kwa Kiwanda Cha Viuadudu Cha TBPL
Habari

Serikali Yapeleka Sh Bil 10 Kwa Kiwanda Cha Viuadudu Cha TBPL

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Lyatuu,Pwani

SERIKALI imeelekeza  jumla ya sh bilioni 10  kwa kiwanda Cha kutengeneza viuadudu Cha TBPL  kilichoko Kibaha mkoani Pwani kwa ajili ya uendelezwaji na uzalishaji wa dawa na viuatilifu mbalimbali  katika mwaka wa fedha 2025/2026.
Mfamasia  Mkuu wa Serikali,Daud Masasi amesema hayo mkoani hapa ikiwa ni uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa kiwanda hicho Cha kipekee kwa Afrika na duniani kwa ujumla ambacho kinaendeshwa nna Shirika la Taifa La Maendeleo (NDC).
Habari Picha 10039
Akizungumza, Masasi amesema upekee wa kiwanda hicho ndio unaosababisha serikali kuongeza Wigo Wa bajeti kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.
Amesema katika miaka minne ya kipindi Cha uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kuanzia 2021/2025 serikali imetoa jumla ya sh bilioni 11.5 ambapo kwa kipindi Cha miaka sita ya mwanzo wakati kiwanda kimeanzishwa fedha zilizotilewa kwa ajili ya kiwanda hicho hazizidi sh bilioni 1.5.
” Ni kiwanda Cha kipekee na serikali inajua umuhimu wake ndio maana kwa bajeti ya mwaka huu zikaelekezwa kiwango hicho Cha fedha ambapo ni sawa na asilimia mia Moja,” amesema Masasi.
Habari Picha 10040
Amesema pamoja na kuongeza bajeti katika kiwanda hicho lakini wameanza uhaulishwaji wa utaalam kwa ndani ya nchi, uwekezaji huo ambao unalenga kupunguza kusambaa kwa ugonjwa wa malaria kwa kiwango kikubwa.
Amesema katika mwaka 2014 ugonjwa wa malaria umepungua kutoka asilimia 14 na kufikia asilimia nane kwa sasa na hiyo inatokana na hamasa ya matumizi ya dawa hizo zinazozalishwa na kiwanda hicho kuongezeka.
Kadhalika amesema tayari Halmashauri zote 184 nchini zimepokea dawa hiyo  ya viuadudu na kuwataka viongozi husika kuendelea kusimamia.
Akizindua maadhimisho hayo,Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda Na Biashara,Dkt Abdallah Hashil amesema Kwa miaka 10 tangu kuanzishwa kwa kiwanda hicho kimekuwa Cha mfano na chenye kuzalisha dawa za aina mbalimbali zaidi ya tatu
Amesema  kwa miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, Serikali imepeleka sh bil 11.5 na Kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha 2025/26 kiwanda kimetengewa jumla ya sh bil 10.
“Ni  nia ya dhati ya serikali kunyanyua kiwanda hicho,

Dhamira ya  kuzalisha dawa ya kuua viuadudu na mpaka sasa Kuna aina tatu za biashara zimeanza kuzalisha…na bidhaa zinazozalishwa hapo  hazina kemikali zinaboresha Maisha ya watanzania,” amesema.
Amesema Dawa zinazozalishwa na kiwanda hicho ni za kuuangamiza mazalia ya wadudu Wa malaria na   zinauzwa mpaka nje ya mipaka ya Tanzania lengo likiwa ni kuhakikisha Malaria inakwisha nchini.
Amezitaja Nchi ambazo zinasambaziwa dawa hizo kuwa ni pamoja na Uganda, Kenya, Msumbiji, Angola, Niger na kwamba karibu asilimia 25 ya dawa inayozaalishwa inauzwa nje ya NCHI ambayo husaidia pia kupatikana kwa fedha ya kigeni.
Habari Picha 10041
Kwa upande wake Mkurugenzi Muendeshaji wa NDC, Dkt Nicholas Shombe amesema hufanya kazi  na watalaam kutoka nchinya Cuba na kwamba bidhaa zinazalishwa  nchini Tanzania kwa asilimia 100 na watanzania.
Amesema mbali ya dawa ya viuadudu vya malaria pia wanazalsiha bidhaa za mbolea ya kisaikolojia isiyokuwa na kemikali na kwamba ni kiwanda Cha watanzania kwa ajili ya watanzania.
Habari Picha 10042

You Might Also Like

Wahamasika Kutumia Mbegu Bora Za Karanga Zilizofanyiwa Utafiti Na TARI

Rais Samia akagua gwaride maalum

Muswada Wa Marekebisho Ya Sheria Za Kazi 2024 Wapitishwa

Tani 27, 550  za ufuta zenye thamani ya bilioni 80 zimeuzwa

Mwenda: Tupo kwa ajili ya kuzitatua changamoto za wananchi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Majaliwa Aipongeza TPHPA kwa Kuhakikisha Usalama wa Chakula Nchini
Next Article Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?