MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Dkt. Mpango: Tumuige Nyerere kwa Kulinda Amani, Uhuru na Maadili ya Taifa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Dkt. Mpango: Tumuige Nyerere kwa Kulinda Amani, Uhuru na Maadili ya Taifa
Habari

Dkt. Mpango: Tumuige Nyerere kwa Kulinda Amani, Uhuru na Maadili ya Taifa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi
MBEYA: MAKAMU wa Rais Dkt. Philip Mpango amewasihi Watanzania kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, kwa kulinda amani, uhuru na mshikamano wa taifa ili kuepuka kupoteza tunu hizo muhimu.
Akizungumza katika kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa na Maadhimisho ya Wiki ya Vijana yaliyofanyika mkoani Mbeya, Dkt. Mpango amesema jamii inapaswa kukemea mmomonyoko wa maadili, rushwa na ufisadi.
Habari Picha 10011
“Vitendo vya mmomonyoko wa maadili na rushwa ni miongoni mwa mambo yanayohatarisha tunu tulizoachiwa na waasisi wetu kama Hayati Mwalimu Nyerere,” amesema Dkt. Mpango.
Aidha, amewasihi wananchi kuhifadhi mazingira kwa kulinda vyanzo vya maji na kupanda miti, akisisitiza kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi wa kuigwa katika maeneo hayo.
Habari Picha 10014
Akizungumzia Mwenge wa Uhuru, Dkt. Mpango amesema ulipoanzishwa ulilenga kuonyesha madhara ya udhalimu wa mkoloni na kuhamasisha amani. “Serikali itaendelea kuenzi falsafa ya Mwenge wa Uhuru katika taifa letu,”.
Kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Vijana, amesema asilimia 77.3 ya Watanzania wana umri chini ya miaka 35, hivyo ni muhimu kwa serikali kutambua mchango wa kundi hilo.
Aliwahimiza vijana kutumia nguvu zao katika ubunifu na maarifa, huku akieleza kuwa Serikali inawaunga mkono. Pia amewataka Wizara ya Elimu Tanzania Bara na Visiwani kutumia kitabu cha Mwenge wa Uhuru alichokizindua kama nyenzo ya kufundishia ili kuendeleza uelewa kwa vijana.
Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, amesema vijana 142,000 kutoka nchi nzima wameshiriki katika midahalo na makongamano yaliyolenga kuwaelimisha.
Habari Picha 10013
Alieleza kuwa uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 umefanyika mkoani Pwani, huku ule wa 2026 ukitarajiwa kufanyika Kusini Pemba na kilele chake kufanyika Rukwa.
Kwa upande wake, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Ismail Ally Ussi kutoka Kaskazini Unguja, amesema waliukabidhi Mwenge huo kwa Dkt. Mpango Aprili 2, 2025 mkoani Pwani. Alibainisha kuwa miradi ya maendeleo 1,382 yenye thamani ya Sh Trilioni 2.87 ilikaguliwa, na yote ilikubaliwa.
Katika misa takatifu ya kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Francisko wa Asizi, Mwanjelwa – Mbeya, Dkt. Mpango aliwaomba Watanzania kuendelea kumuombea Baba wa Taifa ili aendelee kupumzika kwa amani na awe mmoja wa Watakatifu.
Amesema ni muhimu kila mmoja, hususan viongozi, kufuata mfano wa uaminifu wa Baba wa Taifa ambaye alilitakia mema taifa wakati wote.
Kwa niaba ya Serikali, Dkt. Mpango amewashukuru waumini na wananchi wa Mbeya kwa kujitokeza kumuombea Mwalimu Nyerere wakati wa kumbukizi ya miaka 26 tangu kifo chake.
Ibada hiyo iliongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mbeya, Mhashamu Gervas Nyaisonga, aliyesema Mwalimu Nyerere alikuwa mtu wa maadili, haki, huruma, unyenyekevu na uaminifu.
Askofu Nyaisonga alisema Mwalimu aliacha urithi wa kisiasa, muungano wa taifa, mageuzi ya kidemokrasia na Azimio la Arusha la mwaka 1967 lililolenga usawa wa kijamii na kiuchumi. Aidha, alisisitiza kuwa Nyerere alitanguliza elimu, maadili, utamaduni wa Kiswahili, utu na maslahi ya taifa.

You Might Also Like

CCCC Yagusa Wanafunzi Msasani kwa Msaada wa Vifaa vya Shule, Chakula

TARURA Dar Yaendelea Na Ujenzi Wa Miundombinu Ya Barabara Iliyosimama Kutokana Na Mvua

TARI Yaja Na Jawabu 88 Juu Ya Tindikali, Chumvi Kwenye Udongo

Yonaz akabidhi boti ya doria kukabili vitendo vya kiuhalifu

Mdau wa Maendeleo Goryo Ashinda Tuzo Ya Mlipa Kodi Bora

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mwalim: Niko Tayari Kushirikiana na Majaliwa Nikipewa Ridhaa ya Urais
Next Article Mwalim: Lindi, Mtwara Tajiri kwa  Rasilimali, Maskini kwa Uongozi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?