MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ziara ya Kwanza ya Kiongozi wa Juu wa Tanzania Nchini Belarus Yafungua Ukurasa Mpya wa Ushirikiano
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ziara ya Kwanza ya Kiongozi wa Juu wa Tanzania Nchini Belarus Yafungua Ukurasa Mpya wa Ushirikiano
Habari

Ziara ya Kwanza ya Kiongozi wa Juu wa Tanzania Nchini Belarus Yafungua Ukurasa Mpya wa Ushirikiano

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MINSK, BELARUS: KWA mara ya kwanza katika historia ya uhusiano wa kimataifa kati ya Tanzania na Belarus, Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa, amewasili nchini Belarus kwa ziara ya kikazi ya siku nne inayolenga kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili.
Ziara hiyo ya kihistoria, iliyoanza Julai 21 inatarajiwa kuisha 24, 2025 inaashiria mwanzo mpya wa ushirikiano wa kimkakati katika sekta muhimu zikiwemo kilimo, elimu, afya, utalii, uwekezaji, biashara na teknolojia.
Aidha ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania inayolenga kukuza diplomasia ya uchumi.
Waziri Mkuu Majaliwa alipokelewa kwa heshima kubwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Minsk na mwenyeji wake, Naibu Waziri Mkuu wa Belarus,Viktor Karankevich.
Vile vile wengine waliokuwepo ni Waziri wa Uwekezaji Zanzibar,  Sharif Ali Sharif, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Cosato Chumi, pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Urusi,  Fredrick Kibuta.
Majaliwa anatarajiwa kufanya mazungumzo rasmi na Waziri Mkuu wa Belarus, Alexander Turchin, ambapo masuala ya ushirikiano wa maendeleo yatapewa kipaumbele.
Pia atashuhudia utiwaji saini wa Hati za Makubaliano zitakazogusa maeneo ya mashauriano ya kisiasa, kilimo, elimu na biashara.
Mbali na vikao vya serikali kwa serikali Majaliwa atakutana na viongozi wa kampuni na taasisi mbalimbali za Belarus kwa lengo la kuvutia wawekezaji kuja Tanzania. Sekta ya kilimo na teknolojia ya viwanda imewekwa kama maeneo ya kipaumbele katika majadiliano hayo.

You Might Also Like

Udiwani Kata Ya Mbabala Kizungumkuti

Vyama Vya Wafanyakazi Kujadili Hatma Ya Wafanyakazi TAZARA

BoT Yawaalika Wachimbaji Kuwekeza Serikalini, Yatoa Elimu ya Fedha

Homa ya nyani mjadala wa dharura kwa mawaziri wa afya Afrika

Huduma ya Mahakama ya Mwanzo yasogezwa Wilaya ya Ubungo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mapinduzi ya Elimu Geita: Wasichana Wamerudi Shule kwa Kasi
Next Article Rais Samia Atoa Bil. Nne Ujenzi Kiwanda Cha Kuzalisha  Nishati Mbadala  
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Twendeni Tukapige Kura Ya Ukombozi, CHAUMMA Yahitimisha Kampeni
Habari October 28, 2025
Elimu Ya Nishati Safi Ya Kupikia Yawafikia Maofisa Dawati Ngazi Ya Mikoa Na Halmashauri
Habari October 27, 2025
Wananchi wahamasishwa kuandika historia mpya kupitia kura
Habari October 25, 2025
Shibuda: WanaMaswa jitokezeni kupiga kura bila woga
Habari October 25, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?